Mary Kanemba - Bwana Mungu Nashangaa kabisa

Chorus / Description : Bwana Mungu nashangaa kabisa,
Nikifikiri jinsi ulivyo,
Nyota, ngurumo, vitu vyote pia,
Viumbavyo kwa uwezo wako.
hymn Oh God my God when I in awesome God

Bwana Mungu Nashangaa kabisa Lyrics

Bwana Mungu nashangaa kabisa,
Nikifikiri jinsi ulivyo,
Nyota, ngurumo, vitu vyote pia,
Viumbavyo kwa uwezo wako.

Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu,
Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu.


Nikitembea pote duniani,
Ndege huimba nawasikia,
Milima hupendeza macho sana,
Upepo nao nafurahia.

Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu,
Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu.


Nikikumbuka vile wewe Mungu,
Ulivyompeleka mwanao,
Afe azichukue dhambi zetu,
Kuyatambua ni vigumu mno.

Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu,
Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu.

Yesu Mwokozi atakaporudi,
Kunichukua kwenda mbinguni,
Nitaimba sifa zako milele,
Wote wajue jinsi ulivyo.

Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu,
Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu.




Bwana Mungu Nashangaa kabisa Video

  • Song: Bwana Mungu Nashangaa kabisa
  • Artist(s): Mary Kanemba


Share: