Lyrics Page

Mbali Sana

By Beda Andrew

1,757 views Jun 6, 2026 updated

Na na na na... 

Nalikuwa sijiwezi unyonge ulinilemea 

Sikuwa na tumaini ya mbele kuendelea 

Imani ilififia sikuona kabisa

Kama moja ya nyenzo iliyotikisika aah 

Nalikosa tabasamu usoni 

Tegemeo sikuona maishani 

Nikashindwa endelea mbele 

Hali iliyofanya nikwame kule 


Ulikonitoa ni mbali sana 

Ni kweli umenikomboa nashukuru sana 

Ulikonitoa ni mbali sana 

Ukanikomboa na zile laana 


Mbali sana, mbali sana 

Mbali sana nashukuru Bwana 


Uliona haiko shwari mimi kupotea njia 

Sijui namna gani uliwaza ukanihurumia 

Nalifanya nia jangwa mvua kutonyeshe 

Nami mche mbichi maji yalinikaukia 

Shida mateso sina tena, yamewekwa nyuma 

Mimi wa Yesu mwingine sina 

Wa kurudisha nyuma 

Wakati wa kuokolewa umekubalika 

Kwa haki na ushupavu wake ukatibitika 


Ulikonitoa ni mbali sana 

Ni kweli umenikomboa nashukuru sana 

Ulikonitoa ni mbali sana 

Ukanikomboa na zile laana 


Mbali sana, mbali sana 

Mbali sana nashukuru Bwana 


oooh oh oh oooh 

...

Official Video

Save Your Favorites

Create a free account to save songs, build your personal library, and connect with the Zion community.

Create Free Account

Join the Zion Community

Create a free account to save your favorite lyrics, submit song suggestions, and connect with fellow worshippers.

No spam. Unsubscribe anytime.