Mbali Sana Lyrics

By Beda Andrew

Lyrics

Na na na na... 

Nalikuwa sijiwezi unyonge ulinilemea 

Sikuwa na tumaini ya mbele kuendelea 

Imani ilififia sikuona kabisa

Kama moja ya nyenzo iliyotikisika aah 

Nalikosa tabasamu usoni 

Tegemeo sikuona maishani 

Nikashindwa endelea mbele 

Hali iliyofanya nikwame kule 


Ulikonitoa ni mbali sana 

Ni kweli umenikomboa nashukuru sana 

Ulikonitoa ni mbali sana 

Ukanikomboa na zile laana 


Mbali sana, mbali sana 

Mbali sana nashukuru Bwana 


Uliona haiko shwari mimi kupotea njia 

Sijui namna gani uliwaza ukanihurumia 

Nalifanya nia jangwa mvua kutonyeshe 

Nami mche mbichi maji yalinikaukia 

Shida mateso sina tena, yamewekwa nyuma 

Mimi wa Yesu mwingine sina 

Wa kurudisha nyuma 

Wakati wa kuokolewa umekubalika 

Kwa haki na ushupavu wake ukatibitika 


Ulikonitoa ni mbali sana 

Ni kweli umenikomboa nashukuru sana 

Ulikonitoa ni mbali sana 

Ukanikomboa na zile laana 


Mbali sana, mbali sana 

Mbali sana nashukuru Bwana 


oooh oh oh oooh 

...

BEDA ANDREW - MBALI SANA (Official Music Video)SMS SKIZA 7636509 to 811

Now Playing...