Lyrics Page

Shukrani

By Christ Ambassadors

2,155 views Feb 17, 2026 updated

Bwana wangu naomba unisikie  

Nijapo mbele zako 

(Naomba unisikie, naomba unisikie) 

Wimbo wangu siku ya leo si mwingine 

Bali ni wimbo wa shukrani 

(Bwana asante, kwa yote umenitendea) 


Leo naamua kubadili mtazamo wangu Baba 

Unajua muda mwingi nijapo mbele zako 

Huwa naja nikilalamika 

Lakini leo naleta shukrani shukrani 

oh wastahili shukrani Baba 


Muda wowote nikipatwa na jambo baya 

Siwezi sahau kulalamika 

(Kawaida ya mwanadamu, mwepesi wa kulalamika) 

Lakini kwa mazuri muda mwingi huwa nachukulia kawaida 

(Leo nakuja kwa sauti ya shukrani) 


Leo naamua kubadili mtazamo wangu Baba 

Unajua muda mwingi nijapo mbele zako 

Huwa naja nikilalamika 

Lakini leo naleta shukrani shukrani 

oh wastahili shukrani Baba 


Inapendeza kuja mbele zako 

Na sauti za shukrani ewe bwana wangu. 

(Inatupasa wanadamu kukushukuru daima) 

Ni vyema kuwa na shukrani nyingi 

kuliko malalamiko ooh oh. 

(Leo twakuja kwa sauti ya shukrani) 


Leo naamua kubadili mtazamo wangu Baba 

Unajua muda mwingi nijapo mbele zako 

Huwa naja nikilalamika 

Lakini leo naleta shukrani shukrani 

oh wastahili shukrani Baba 

Official Video

Save Your Favorites

Create a free account to save songs, build your personal library, and connect with the Zion community.

Create Free Account

Join the Zion Community

Create a free account to save your favorite lyrics, submit song suggestions, and connect with fellow worshippers.

No spam. Unsubscribe anytime.