Lyrics Page

Mateso

By Erick Smith

1,788 views Jun 6, 2026 updated

Kwa kupigwa kwako tumepona 

Msalabani yote yamekwisha 

Kwa kupigwa kwako tumepona 

Msalabani yote yamekwisha 


Nikikumbuka mateso yake Yesu 

Alivyoteseka pale msalabani.

Fimbo, misumari, taji ya miba 

Mkuki ubavuni na kutemewa mate. 


Mateso yake Yesu ilikuwa ni huzuni 

Mwana wa Mungu kafa bila hatia yeyote 

Ili mimi na wewe tuhesabiwe haki 

(rudia) 


Wakamkamata Yesu kama mwizi 

Na kumdharau Yesu mwana wa Mungu. 

Wakamkamata kama mwizi 

Wakumdharau Bwana mwana wa Mungu. 

Wakadhani kuwa ndio mwisho 

Kumbe ndio mwanzo wa wokovu wangu 

Kumbe ndio mwanzo wa wokovu wetu. 


Mateso yake Yesu ilikuwa ni huzuni 

Mwana wa Mungu kafa bila hatia yeyote 

Ili mimi na wewe tuhesabiwe haki 

(rudia) 


Akasulubiwa Yesu Ju ya msalaba 

Akasema Baba, Baba oh wasamehe 

Kwani hawajui walitendalo oh ooh 

Ndipo Bwana wangu akakata roho 

Ndipo Bwana wangu akakata roho  


Kwa kupigwa kwako tumepona 

Msalabani yote yamekwisha 

Kwa kupigwa kwako tumepona 

Msalabani yote yamekwisha 


Mateso yake Yesu ilikuwa ni huzuni 

Mwana wa Mungu kafa bila hatia yeyote 

Ili mimi na wewe tuhesabiwe haki

Official Video

Save Your Favorites

Create a free account to save songs, build your personal library, and connect with the Zion community.

Create Free Account

Join the Zion Community

Create a free account to save your favorite lyrics, submit song suggestions, and connect with fellow worshippers.

No spam. Unsubscribe anytime.