Lyrics Page

Mungu Hapokei Rushwa

By Goodluck Gozbert

1,819 views Jun 6, 2026 updated

Uzuri ni kwamba Mungu hapokei rushwa 

Uzuri ni kwamba Mungu hapokei rushwa 

Angepewa mabilioni tungetupwa mbali sana 

Angepewa mabilioni tungetupwa mbali sana 


Uzuri ni kwamba Mungu hapokei rushwa 

Uzuri ni kwamba Mungu hapokei rushwa 

Angepewa mabilioni tungetupwa mbali sana 

Angepewa mabilioni tungetupwa mbali sana 


Na wengine tuna damu mbaya  

Mabifu kama yote

Mtu hujamkosea anatamani ufe 

Wengine Bwana wee tulipewaga sura mmh 

Mtu akikuona akalinganisha hufanani 

Wewe unadhani angepewa oxygeni eeh 

Yangu angeminya, angeminya nifie mbali 

Wewe unadhani angepewa kesho yako eeh

Kwanza angefinya angefinya, ufie mbali 

Ila Mungu wee eeeh hajui kukosea 

Ametupa thamani tulioitwa vikaragosi 

Ila Mungu wee eeeh mwingi wa huruma

Ametupa vicheko, vicheko bila manoti 


Uzuri ni kwamba Mungu hapokei rushwa 

Uzuri ni kwamba Mungu hapokei rushwa 

Angepewa mabilioni tungetupwa mbali sana 

Angepewa mabilioni tungetupwa mbali sana 


Mfano jitu lipate, kama za Laiza

Lingetuchakaza vibaya, au lipate kama za Dangote 

Lipewe kuamua kesho yako eeh 

Wengine baba zetu walala hoi 

Wengine mama zetu hohehahe 

wengine familia zetu choka mbaya 

Wengine ndio kabisa mayatima 

Hakuna anayetujua wala hatuna connection mmh 

Kusema sababu ni elimu mbona wasomi kibao ni jobless 

Tumewekwa mahali kwa neema ya Mungu 

Tunavuka mapito kwa neema ya Mungu 

Huyu Mungu wee eeh hajui kukosea 

Ametupa thamani tulioitwa vikaragosi 

Ila Mungu wee eeeh mwingi wa huruma 

Ametupa vicheko, vicheko bila manoti 


Uzuri ni kwamba Mungu hapokei rushwa 

Uzuri ni kwamba Mungu hapokei rushwa 

Angepewa mabilioni tungetupwa mbali sana 

Angepewa mabilioni tungetupwa mbali sana 


Uzuri ni kwamba Mungu hapokei rushwa 

Uzuri ni kwamba Mungu hapokei rushwa 

Angepewa mabilioni tungetupwa mbali sana 

Angepewa mabilioni tungetupwa mbali sana 

Official Video

Save Your Favorites

Create a free account to save songs, build your personal library, and connect with the Zion community.

Create Free Account

Join the Zion Community

Create a free account to save your favorite lyrics, submit song suggestions, and connect with fellow worshippers.

No spam. Unsubscribe anytime.