Nipe Lyrics

By Goodluck Gozbert

Lyrics

Hata nikiwa sina chakula 

Isinifanye kusahau 

Ulinilisha nikasaza 

Hata nikiwa sina mavazi 

Isinifanye nifukuru 

Na kusahau umeniweka hai 

Ona wapo marafiki 

Wanakosa kula na kuvaa 

Hawalalamiki, wanakushukuru tu 

Mimi eh, nilikupa nini Baba 

Cha kunipa kibali

Kwa siku zilizofurahisha? 


Taabu kidogo zisinifanye nikusahau 

Umeshatenda mengi – nikiwa hapa 

Shida itapita, bado kidogo 

Ikiwa nitachoka niiunue 


Refrain:

Nipe kukumbuka wema  

Nipe kukumbuka wema 

Nipe kukumbuka wema 

Nipe kumbuka wema wako 


Hata kwenye bonde hili la mauti 

Nakumbuka nilikuita, 

Na wewe ukaitika Baba 

Kutegemea akili zangu, na mawazo yangu 

Kutanifanya niendelee 

niendelee kulalamika 

Kuna kipindi najisahau 

na kujivunia mafanikio 

Wengine naona takataka 

Nikumbushe mi ni mtu tu 

na dunia tunapita 

Uhai wangu si faida bila wewe 


Mungu wewe ni mkuu 

kuliko vile nakutazama Baba 

Unisamehe, unisamehe 

Kuna nyakati nadhani 

hii dunia labda ni ya ushindani 

Natumia akili zangu za ndani 

Ila bado nashindwa kuendelea 

Nikimbushe nisidhani 

Wakifanikiwa tuna upinzani 

Nifundishe kuwaombea amani 

Na utatenda kwa wakati 


Na ikiwa Kama nikisahau 

Unikumbushe mi mtoto wako 


Nipe kukumbuka wema  

Nipe kukumbuka wema 

Nipe kukumbuka wema 

Nipe kumbuka wema wako 


Now Playing...