Nyakati Lyrics

By Goodluck Gozbert

Lyrics

Unaona kama kila unachogusa kimeharibika 

UJasiri wa kusema tena umetoweka 

Maana kila unalosema wewe kama unakosea 

Umechanganyikiwa ni Mungu ajua unayopitia 

Na ukisema ueleze wengi kwao ni furaha 

Wewe mwombe Mungu ubaki kimya 

Na mengi umevumilia moyo umenyong'onyea 

Hapo ulipo sasa ng'ang'ania tena 

Na Mungu hajaruhusu jaribu kuliko uwezo wako. 

Imani nusu ongeza utashinda. 

Mungu hatoruhusu ufe kabla ya baraka zako 

Imani nusu ongeza utashinda. 


Zipo nyakati za furaha 

Nawe utacheka tena usijali, Mungu yupo nawe. 

Zipo nyakati za furaha 

Nawe utacheka tena usijali, Mungu yupo nawe.  


Oooh! Mmmh! 

Moyo wako una majeraha haufai 

Tena unasubiri kauli ya mwisho ya Mungu 

Wapo wanaojua we huna mtoto wa kejeli 

Wanaulizaga ana umri gani? 

Tena wanaojua umefukuzwa kazi 

Kwa kejeli wanaulizaga bosi wako yupo? 

Ila nakwambia hayatodumu, ni nyakati tu. 

Ila nakwambia hayatodumu, ni nyakati tu, 

Hautobaki hapo haya ni mapito jipe moyo 

Tazama juu mwombe Mungu ujasiri 

Ni mapito tu jipe moyo mkuu  

Mungu hajaruhusu jaribu kuliko uwezo wako 

Imani nusu ongeza utashinda. 

Mungu hatoruhusu ufe kabla ya baraka zako 

Imani nusu ongeza utashinda.  


Zipo nyakati za furaha 

Nawe utacheka tenA, usijali Mungu yupo nawe. 

Zipo nyakati za furaha 

Nawe utacheka tena, usijali Mungu yupo nawe.  


Hata wakizusha maneno ya uongo 

Wakakwambia umemuasi Mungu 

Uh ni sawa hawajui unakopita 

Wakaja na unabii wakasema 

umefika mwisho wako wewe 

Ni sawa hawajui unakopita oooh! 

Wakainuka ndugu wa karibu, wakakusema ovyo ovyo 

Ni sawa hawajui unakopita 

Ikawa kila kitu ni kimya marafiki ni kimya ooh 

Ni sawa hawajui unakopita 

Kama ndoa ni yako lakini ndani ni uadui 

Ni sawa hawajui unakopita 

Ila 


Zipo nyakati za furaha 

Nawe utacheka tenA, usijali Mungu yupo nawe. 

Zipo nyakati za furaha 

Nawe utacheka tena, usijali Mungu yupo nawe.  

Zipo nyakati za furaha 

Nawe utacheka tenA, usijali Mungu yupo nawe.  


Laa laa lala!

END

Now Playing...