Lyrics Page

Nafasi Nyingine

By Joel Lwaga

2,560 views Jun 6, 2026 updated

Mavumbi umenivuta yote 

Habari umebadili yote 

Machozi umenifuta yote 

Aibu umeondoa yote 


Umeniita mwana niliyekuwa mtumwa 

Umenisimamisha katika wingi wa neema 

Na umeniketisha mahali pa juu sana 

Ninaucheka wakati uliyopita 

Nikiufurahia ule ujao 

Ninaucheka wakati uliyopita 

Nikiufurahia ule ujao 


Baba umenipa nafasi nyingine 

Unanipenda tena bila kukoma (nafasi nyingine) 

Neema yako imeniinua tena (nafasi nyingine) 

Umenipa tena bila kuchoka (nafasi nyingine)

Wa neema Mungu wa neema 

Wa neema neema aaah aah 


Madakari walisema sitapona tena 

Walimu walisema nitafeli 

Ndugu na jamaa walisema nimeshindikana 

Na kumbe kwako wee waniwazia mema 

Umri uliposogea walisema ndoa si fungu langu 

Nilipofiwa na mpendwa walisema siwezi tena 

Baada tu ya kufilisika sikuona wakuniombea 

Na kumbe ndani yao walifurahi niliyopitia 

Ninaucheka wakati uliyopita 

Nikiufurahia ule ujao 

Ninaucheka wakati uliyopita 

Nikiufurahia ule ujao 


Baba umenipa nafasi nyingine 

Unanipenda tena bila kukoma (nafasi nyingine) 

Neema yako imeniinua tena (nafasi nyingine) 

Umenipa tena bila kuchoka (nafasi nyingine)

Wa neema Mungu wa neema 

Wa neema neema aaah aah 


Official Video

Save Your Favorites

Create a free account to save songs, build your personal library, and connect with the Zion community.

Create Free Account

Join the Zion Community

Create a free account to save your favorite lyrics, submit song suggestions, and connect with fellow worshippers.

No spam. Unsubscribe anytime.