Nivushe Lyrics

By Joel Lwaga

Lyrics

Mambo ni mengi nimepitia 

Machozi ni mengi nimelia 

Hata kicheko ni cha bandia 

Inafunika mengi ninayopitia 


Ila najua iko yako 

Ya pili isiyo na haya majuto 

Tena si ya ulimwengu ule uchao 

Ila ni ya ulimwengu huu wa leo 


Eeh Bwana nivushe nivushe ng'ambo 

Nivushe ng'ambo (Nivushe ng'ambo)

Eeh Bwana nivushe nivushe ng'ambo 

Nivushe ng'ambo (Nivushe ng'ambo)


Maana najua sikusudi lako niishi hapa 

Maana najua si kusudi lako nikwame

Maana najua si kusudi lako niaibike 

Maana najua si kusudi lako nianguke


Sasa nyosha mkono wako univushe ng'ambo ya pili 

Bwana nimefika mwisho wa uwezo wangu wa akili

Nimekuja ishiya leo mazuri uliyoniahidi 

Nisiyaone kwa mbali niyashike na kuyamiliki


Nivushe nivushe nivushe ng'ambo 

Nivushe ng'ambo (Nivushe ng'ambo)

Eeh Bwana nivushe nivushe ng'ambo 

Nivushe ng'ambo (Nivushe ng'ambo)

Now Playing...