Lyrics Page

Wanitazama

By Joel Lwaga

1,373 views Jun 6, 2026 updated

Mkono wako umenishika

Fimbo yako yaniongoza

Gongo lako lanifariji

Umenisitiri umenifanya hodari

Uliliona chozi langu la ndani

Ukalifuta na kunipa amani

Unyonge wangu haukukuweka mbali

Ukaniinua na kunipa dhamani


Eeh Bwana, wanitazama

Baba, baba Mungu usielala

Wanitazama, wanitazama

Baba, baba Mungu usiyechoka


Mi ni mboni yako 

(Yesu wee, Yesu wee)

Jicho lako

Yesu wee, Yesu wee

Mi ni mboni yako 

(Yesu wee, Yesu wee)

Jicho lako

(Yesu wee, Yesu wee)


Akili zangu Zilifika mwisho

Na kuona Mungu hunitazami taabuni

Na wanadamu

Wakapata cha kusema kuwa 

Mungu wangu hayupo tena nami


Nilipoona ni mwisho

Wewe ukatangaza mwanzo

Nilipodhani ni pigo

Kumbe ni lako kusudio

Kilipozidi kilio

Wewe ukaleta kicheko

Ukadhihirisha kwa macho

Wewe ni langu kimbilio


Uliliona chozi langu la ndani

Ukalifuta na kunipa amani

Unyonge wangu haukukuweka mbali

Ukaniinua na kunipa dhamani

Eeh Bwana, wanitazama

Baba, baba Mungu usielala

Wanitazama, wanitazama

Baba, baba Mungu usiechoka


Eeh Bwana, wanitazama

Baba, baba Mungu usielala

Wanitazama, wanitazama

Baba, baba Mungu usiyechoka


Mi ni mboni yako 

(Yesu wee, Yesu wee)

Jicho lako

Yesu wee, Yesu wee

Mi ni mboni yako 

(Yesu wee, Yesu wee)

Jicho lako

(Yesu wee, Yesu wee)


Uliliona chozi langu la ndani

Ukalifuta na kunipa amani

Unyonge wangu haukukuweka mbali

Ukaniinua na kunipa dhamani

Eeh Bwana 

Official Video

Save Your Favorites

Create a free account to save songs, build your personal library, and connect with the Zion community.

Create Free Account

Join the Zion Community

Create a free account to save your favorite lyrics, submit song suggestions, and connect with fellow worshippers.

No spam. Unsubscribe anytime.