Lyrics Page

Namwandama Bwana - Amini Utii 17

By Magena Main Youth Choir

1,227 views Jun 6, 2026 updated

Namwandama Bwana kwa alilonena,

Njia yangu huning'azia;

Nikimridhisha atanidumisha

Taamini nitii pia.


Amini utii, njia pweke ni hii

Ya furaha kwa yesu, amini ukatii


Giza sina kwangu wala hata wingu

Yeye mara huviondoa

Woga wasiwasi, sononeko basi.

Huamini nitii pia.


Amini utii, njia pweke ni hii

Ya furaha kwa yesu, amini ukatii


Masumbuko yote, sikitiko lote;

Kwa mapenzi hunilipia,

Baa, dhara, dhiki, vivyo hubariki,

Taamini nitii pia.


Amini utii, njia pweke ni hii

Ya furaha kwa yesu, amini ukatii


Mimi sitajua raha sawasawa

Ila yote yesu kumpa;

Napata fadhili na radhi kamili,

Taamini nitii pia.


Amini utii, njia pweke ni hii

Ya furaha kwa yesu, amini ukatii


Nitamfurahisha na kumtumaini,

Majumbani na njia-njia;

Agizo natenda; nikitumwa hwenda,

Huamini nitii pia


Amini utii, njia pweke ni hii

Ya furaha kwa yesu, amini ukatii

Save Your Favorites

Create a free account to save songs, build your personal library, and connect with the Zion community.

Create Free Account

Join the Zion Community

Create a free account to save your favorite lyrics, submit song suggestions, and connect with fellow worshippers.

No spam. Unsubscribe anytime.