Lyrics Page

Asante

By Natasha Lisimo

1,825 views Jun 10, 2026 updated

Ni rahisi moyo lawama linapotokea mbaya 

Ninasahau hayo yote ni mpango wako 

Ninapata shida kichwani ninachanganyikiwa 

Nikumbushe wema wako, wakati wote nikuabudu 

Nikusifu kwa hali zote nisiende mbali nawe 



Wakati wote niwe nawe (Baba) 

Machozi yangu yafute (Mungu)

Wakati wote niwe nawe (Bwana) 

Machozi yangu yafute (Mungu)


Ni wewe ndiwe mfariji wapekee 

Baba wa yatima, mume wa wajane 

Niwezeshe kustahimili kiangazi na masika 

Pepo mbaya na mzuri pale unaponipitia 

Nisimame mbele zako milele milele 

Nishike na mkono wako daima daima 

Maana kila litokalo wewe umepanga litokee 

Sio kwamba nia yako tupotee ila tuzidishe imani 


Wakati wote niwe nawe (Baba) 

Machozi yangu yafute (Mungu)

Wakati wote niwe nawe (Bwana) 

Machozi yangu yafute (Baba) 


Asante kwa yote (Baba) 

Nimekuwa jasiri (Asante) 

Asante kwa yote mema 

(asante kwa yote) 

Kwa utukufu wako (asante) 

Asante Baba (asante) 

Pokea moyo shukurani (asante kwa yote) 

Oh Baba (asante ) 

Nakushukuru kwa njia zako (asante) 

Nakushukuru kwa matendo yako (asante)

Official Video

Save Your Favorites

Create a free account to save songs, build your personal library, and connect with the Zion community.

Create Free Account

Join the Zion Community

Create a free account to save your favorite lyrics, submit song suggestions, and connect with fellow worshippers.

No spam. Unsubscribe anytime.