Lyrics Page

Achana Nao

By Sei Sisters

3,181 views Jun 6, 2026 updated

Kazi ya kupigana na watu wa Mungu achana nayo 

Wapakwa mafuta ni wateule achana nao 

Vita vyao ni Mungu mwenyewe anawapigania eeh 

Wamezingirwa na moto cheza mbali nao 


Achana nao ah, Achana nao eeh 

Wapakwa mafuta ni wateule achana nao 

Achana nao ah, Achana nao eeh eh 

Walioitanishwa kwa jina la Baba achana nao 


Sauli kwa unafiki aliokuwa nayo 

Alipanga vita kinyume na mtu wa Mungu Daudi 

Hakujua vita vya Daudi ni vyake Mungu eeh

Mungu alimleta Sauli hadi mikononi mwa Daudi 

Daudi alikata vazi la Sauli kisha akamuonyesha 

Akamwambia tazama ningetaka ningekuangamiza ah 

Sauli kutazama akapiga magoti akatoa machozi 

Hapo akatambua wapakwa mafuta achana nao 

Vita vyao ni Mungu mwenyewe anawapigania ah eh 


Achana nao ah, Achana nao eeh 

Wapakwa mafuta ni wateule achana nao 

Achana nao ah, Achana nao eeh eh 

Walioitanishwa kwa jina la Baba achana nao 


Kuna watu wameitwa wamepakwa mafuta 

Kwa kazi ya Bwana wamejitoa kwa hali na mali 

Lakini bado kukataliwa kushushwa moyo 

kuonewa bure, kushushwa chini, kudharauliwa 

Ewe usife moyo, kwani tunaye Mungu 

Ewe usife moyo, kwani tunaye Mungu 

Vita vyetu ni Mungu mwenyewe atupigania 


Achana nao ah, Achana nao eeh 

Wapakwa mafuta ni wateule achana nao 

Achana nao ah, Achana nao eeh eh 

Walioitanishwa kwa jina la Baba achana nao


Ninamwita Mungu wa akina Shadrack akupiganie 

Kwenye moto ya majaribu usichomeke 

Ninamwita Mungu wa Danieli akupiganie wewe 

Afunge midomo ya adui zako uishi salama 

Ninamwita Mungu wa Israeli akupiganie eeh 

Afanye njia mahali ambapo hapana njia 

Wapendwa msife moyo kwani tunaye Mungu 


Achana nao ah, Achana nao eeh 

Wapakwa mafuta ni wateule achana nao 

Achana nao ah, Achana nao eeh eh 

Walioitanishwa kwa jina la Baba achana nao 


Achana nao ah, Achana nao eeh 

Wapakwa mafuta ni wateule achana nao 

Achana nao ah, Achana nao eeh eh 

Walioitanishwa kwa jina la Baba achana nao


Official Video

Save Your Favorites

Create a free account to save songs, build your personal library, and connect with the Zion community.

Create Free Account

Join the Zion Community

Create a free account to save your favorite lyrics, submit song suggestions, and connect with fellow worshippers.

No spam. Unsubscribe anytime.