Lyrics Page

Unaniona

By Walter Chilambo

1,865 views Jun 6, 2026 updated

Kama Mungu angechagua watu wake 

Mimi singekuwepo duniani 

Kama Mungu angechagua watakatifu 

Mimi singekuwepo duniani 


Mimi binadamu wala si malaika 

Mengi ninakosea na kukuchukiza 

Ninafanya mambo yasiyostahili 

Nimevuruga-vuruga mipango yako 

Wanihurumia, 


Mbele ya macho ya wanadamu 

Nilikuwa nikijificha 

Kumbe wewe waniona 

Kwa Kujifanya (mtakatifu) tena (mkarimu) 

Nilikuwa (mnyenyekevu tena mpole sana) 

Kwa Kujifanya (mtakatifu) tena (mkarimu) 

Kwenye ibada (mnyenyekevu tena mpole sana)


Kumbe Mungu aniona, macho yako yanitazama 

Sikio lako lanisikia, siwezi jificha aah 

Kumbe Mungu aniona, macho yako yanitazama 

Sikio lako lanisikia, siwezi jificha aah 


Sasa nimetambua mbivu na mbichi ni zipi 

Sasa ninaelewa njia salama ni wapi 

Na nimejua bila ya wewe sifiki 

Hata nikila pasipo neno lako sishibi 

Neema yako (ila kwa neema yako) 

Upendo wako (ila kwa upendo wako) 

Na rehema zako zimenihimarisha tena 


Mbele ya macho ya wanadamu 

Nilikuwa nikijificha 

Kumbe wewe waniona 

Kwa Kujifanya (mtakatifu) tena (mkarimu) 

Nilikuwa (mnyenyekevu tena mpole sana) 

Kwa Kujifanya (mtakatifu) tena (mkarimu) 

Kwenye ibada (mnyenyekevu tena mpole sana) 


Kumbe Mungu aniona, macho yako yanitazama 

Sikio lako lanisikia, siwezi jificha aah 

Kumbe Mungu aniona, macho yako yanitazama 

Sikio lako lanisikia, siwezi jificha aah 

Official Video

Save Your Favorites

Create a free account to save songs, build your personal library, and connect with the Zion community.

Create Free Account

Join the Zion Community

Create a free account to save your favorite lyrics, submit song suggestions, and connect with fellow worshippers.

No spam. Unsubscribe anytime.