Chorus / Description :
(When We Walk with the Lord / Trust and Obey) 17
Namwandama Bwana kwa alilonena,
Njia yangu huning'azia;
Nikimridhisha atanidumisha
Taamini nitii pia.
Amini utii, njia pweke ni hii
Ya furaha kwa yesu, amini ukatii
Namwandama Bwana kwa alilonena,
Njia yangu huning'azia;
Nikimridhisha atanidumisha
Taamini nitii pia.
Amini utii, njia pweke ni hii
Ya furaha kwa yesu, amini ukatii
Giza sina kwangu wala hata wingu
Yeye mara huviondoa
Woga wasiwasi, sononeko basi.
Huamini nitii pia.
Amini utii, njia pweke ni hii
Ya furaha kwa yesu, amini ukatii
Masumbuko yote, sikitiko lote;
Kwa mapenzi hunilipia,
Baa, dhara, dhiki, vivyo hubariki,
Taamini nitii pia.
Amini utii, njia pweke ni hii
Ya furaha kwa yesu, amini ukatii
Mimi sitajua raha sawasawa
Ila yote yesu kumpa;
Napata fadhili na radhi kamili,
Taamini nitii pia.
Amini utii, njia pweke ni hii
Ya furaha kwa yesu, amini ukatii
Nitamfurahisha na kumtumaini,
Majumbani na njia-njia;
Agizo natenda; nikitumwa hwenda,
Huamini nitii pia
Amini utii, njia pweke ni hii
Ya furaha kwa yesu, amini ukatii