Yesu Kwetu ni Rafiki
By Nuru Kitambo
Lyrics
1.Yesu kwetu ni rafiki, Huambiwa haja pia;
Tukiomba kwa Babaye Maombi asikia;
Lakini twajikosesha, Twajitweka vibaya;
Kwamba tulimwomba Mungu Dua angesikia.
2. Una dhiki na maonjo? Una mashaka pia.
Haifai kufa moyo, Dua atasikia
Hakuna mwingine mwema Wa kutuhurumia;
Atujua tu dhaifu; Maombi asikia.
3. Je, hunayo hata nguvu, Huwezi kuendelea,
Ujapodharauliwa Ujaporushwa pia, Watu wange kudharau,
Wapendao dunia, Hukwambata mikononi, Dua atasikia.
Nuru Kitambo - Yesu Kwetu Ni Rafiki
Song Information
- Artist
- Nuru Kitambo
- Released
- November 3, 2014
- Genre / Category
- praise
- Views
- 2,583