Annastacia Mukabwa - Watangoja Sana

Chorus / Description : watangoja sana
Wanaongoja kuanguka kwako
Wanaongoja kushindwa kwako
Wanaongoja umuache Yesu
Wanaongoja uharibikiwe wacheke

Waambie pole, pole pole
Ninaye Yesu, ninaye mwokozi
Waambie pole, pole pole
Watangoja sana

Watangoja Sana Lyrics

watangoja sana 
Wanaongoja kuanguka kwako 
Wanaongoja kushindwa kwako 
Wanaongoja umuache Yesu 
Wanaongoja uharibikiwe wacheke 

Waambie pole, pole pole 
Ninaye Yesu, ninaye mwokozi 
Waambie pole, pole pole 
Watangoja sana 

Yesu alipokufa akazikwa kaburini 
Wengi walicheka sana Wengine walisema 
?Si unajifanya ni mwana wa Mungu? 
?Hebu jifufue tukuone? 
Waliweka na walinzi walinde kaburi 
Ili Yesu asifufuke 
Waliweka na jiwe kubwa, pale kaburini 
Ili Yesu asifufuke, Siku ya tatu ilipofika 
Walinzi walishangaa, Yesu hayupo kaburini 
Siku ya tatu ilipofika, Walinzi walishangaa 
Yesu hayupo kaburini, amefufuka 

watangoja sana 
Wanaongoja matanga yako,
Wanaongoja urudiwe kwenyu nani wateleza 
Wanaongoja ufutwe kazi wacheke 

Waambie, pole, pole, pole 
Ninaye yesu sibabaiki mimi nalindwa na Jehova 
Ananipigia vita, Watangoja sana

Eh ni Mungu pekee yake
Analalamishwa juu yako 
Hakuna silaha itainuka 
Kinyume chako ifanikiwe
Maneno ya watu yasikuvunje moyo 
Tegemea we utashinda, utashinda 

watangoja sana 
Wanaongoja kuanguka kwako 
Wanaotaka ndoa yako ivunjike wacheke 
Wanaotamani ufilisike wacheke 
Wanaosema utakufa bila kuzaa mama 

Waambie pole, pole, pole 
Ninalindwa na jeshi la mbinguni 
Wambie, pole, pole, pole 
Watangoja sana 

watangoja sana, Wanasema hutaolewa 
Wanasema utashindwa na elimu 
Wanaofitini ushukishwe cheo 
Wanaosema huwezi fika popote 

Waambie pole, pole pole 
Wanaotabiri, wanaokuwazia 
Watangoja sana 
Ninaye Yesu, nasonga mbele 
Nyuma sirudi tena 
Watangoja sana 

BweniEve Productions

Watangoja Sana Video

  • Song: Watangoja Sana
  • Artist(s): Annastacia Mukabwa
  • Album: Watangoja Sana - Single
  • Release Date: 01 Feb 2021
Watangoja Sana Audio Preview: Download / Stream : Amazon Music / iTunes


Share: