Shujaa Wa Msalaba Lyrics

By Rose Muhando

Lyrics

Nainua macho yangu

Nitazame mbinguni

Moyo Wangu unasema niwe Mungu wangu

Kilindi cha moyo Wangu kimefurika neno lako

Wacha nikwabudu ewe Mungu wangu

kwenye kiti cha rehema, kumejawa utukufu wako

Wacha nikwabudu ewe Mungu wangu

kileleni pa msalaba, kumeandikwa jina lako

Simba wa wayahudi ndiwe Mungu waangu


Shujaa wa msalaba, umeinuliwa juu.

Wacha nikwabudu ewe Mungu wangu 


Shujaa wa msalaba, umeinuliwa juu.

Wacha nikwabudu ewe Mungu wangu 


Wingu la uwepo wako, limeshuka kwa watu wako 

Utukufu una wewe ewe Mungu wangu 

Nguvu zilizo shinda kaburi 

zionekane kwa watu wako. 

Nani kama wewe ewe Mungu wangu 

Makovu na misumari yatangaza utukufu wako Baba 

Wacha nikwabudu ewe Mungu wangu 

Taji ya miba na misumari 

Yatangaza uwezo wako 

Mfalme wa wafalme ndiwe Mungu wangu 


Shujaa wa msalaba, umeinuliwa juu 

Wacha nikwabudu ewe Mungu wangu  


Siku ya msiba wangu 

Nitalitaja jina lako 

Bwana wa Mabwana ndiwe Mungu wangu 

Sitanyamaza mchana sitakaa kimya usiku 

Wacha nikusifu ewe Mungu wangu 

Nguvu na uweza wako ziko mikononi mwako 

Nani kama wewe ewe Mungu wangu 

Ulipewa jina jipya lipitalo majina yote 

Bwana wa mabwana ewe Mungu wangu 


Shujaa wa msalaba, umeinuliwa juu 

Wacha nikwabudu ewe Mungu wangu  


Shujaa wa msalaba, umeinuliwa juu 

Wacha nikwabudu ewe Mungu wangu  


Shujaa wa msalaba, umeinuliwa juu 

Wacha nikwabudu ewe Mungu wangu  


"Rose Muhando Shujaa Wa Msalaba"

Now Playing...