Kazi yangu ikiisha, nami nikiokoka
Na kuvaa kutokuharibika, Nitamjua Mwokozi nifikapo ng?amboni
Atakuwa wa kwanza kunilaki.
Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso;
Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari.
Furaha nitapata nikiona makao Bwana aliyotuandalia;
Nitamsifu mwokozi kwa rehema na pendo
Vilivyonipa pahali Mbinguni.
Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso;
Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari.
Nao waliokufa katika Bwana Yesu, Nitawaona tena huko juu;
Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni, Nataka kumwona Mwokozi kwanza.
Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso;
Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari.
Milangoni mwa mji Bwana atanipitisha,
Pasipo machozi wala huzuni.
Nitauimba wimbo wa milele;
lakini Nataka kumwona Mwokozi kwanza.
Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso;
Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari.
# I will Know Him
kazi yangu ikiisha nami nikiokoka - Nitamjua
Emachichi's song 'Kazi yangu ikiisha, nitamjua' is a Swahili gospel song about the hope of meeting Jesus face to face after finishing life's work. The lyrics express anticipation of seeing the Savior in heaven, recognizing Him by the nail prints in His hands. The song also speaks of joy in the eternal home prepared by God, reunion with departed believers, and the absence of sorrow at heaven's gates. It emphasizes that above all, the singer longs to see Jesus first. The repeated chorus 'Nitamjua' (I will know Him) underscores the certainty of this future encounter.