1.Yesu kwetu ni rafiki, Huambiwa haja pia;
Tukiomba kwa Babaye Maombi asikia;
Lakini twajikosesha, Twajitweka vibaya;
Kwamba tulimwomba Mungu Dua angesikia.
2. Una dhiki na maonjo? Una mashaka pia.
Haifai kufa moyo, Dua atasikia
Hakuna mwingine mwema Wa kutuhurumia;
Atujua tu dhaifu; Maombi asikia.
3. Je, hunayo hata nguvu, Huwezi kuendelea,
Ujapodharauliwa Ujaporushwa pia, Watu wange kudharau,
Wapendao dunia, Hukwambata mikononi, Dua atasikia.
Lyrics Page
Yesu Kwetu ni Rafiki
3,434 views
Jun 6, 2026 updated