Peter Blessing - Nasubiri Bado

Chorus / Description : Mwenyezi mimi nasubiri bado (mwenyezi)
Nasubiri bado (mwenyezi)
Nasubiri bado nangoja kwako (mwenyezi)
Nasubiri bado (mwenyezi)

Nasubiri Bado Lyrics

Kutwa nzima imepita nikiwa ata sina cha mfukoni 
Naumia hakika kwani ata marafiki nao siwaoni 
Kwenye wingu la giza sijapata ata faraja tumboni 
Koroboi ndo stima namweleza yule unayetoka moyoni 
Maisha haya kizunguzungu ni wapi tena sina pakutorokea 
Kwenye giza sioni nuru ni nini chanzo nabaki nikijiongelea 
Kama namwona mamangu uchochole ndio wimbo na ndo kikwazo 
Pekee yangu kwa hakika naangaziwa sana 
Machozi ndo yangu hata kunivika cha chini ndio langu pato 
Eeeh mola wangu eeeh eeh 

Mwenyezi mimi nasubiri bado (mwenyezi) 
Nasubiri bado (mwenyezi) 
Nasubiri bado nangoja kwako (mwenyezi) 
Nasubiri bado (mwenyezi) 
Nasubiri bado (mwenyezi) 
Nasubiri bado nangoja kwako (mwenyezi) 

Mbona mawazo yangu ndo hivo katu sichoki kufikiria 
Masikini moyo wangu 
Mzigo wangu ndo mzito sina ata wa kunisaidia 
Naja kwako mola wangu maumivu yangu yaokolee 
Toka zama sichoki kusota dili zangu zakutege 
Mara napata saa zingine nakosa nyumbani nategemewa 
Wamechoka wa kunikopesha wazidi niombea wasikate tamaa 
oooh ooh oooh 
Kama kufunga sio mwanzo ni mtindo mpaka nashindwa nini ndo chanzo 
Ndio maana nimeandika wimbo 
Matatizo yasiyokosa likizo kilio ndio yangu mtindo 
Ni maji yamefika kwa shingo aaih 
Kama namwona mamangu uchochole ndio wimbo na ndo kikwazo 
Pekee yangu kwa hakika naangaziwa sana 
Machozi ndo yangu hata kunivika cha chini ndio langu pato 
Eeeh mola wangu eeeh eeh 

Mwenyezi mimi nasubiri bado (mwenyezi) 
Nasubiri bado (mwenyezi) 
Nasubiri bado nangoja kwako (mwenyezi) 
Nasubiri bado (mwenyezi) 
Nasubiri bado (mwenyezi) 
Nasubiri bado nangoja kwako (mwenyezi) 

Kupambana kidume sichoki 
Sala zangu nitume sichoki 
Siwasikizi wengine sichoki 
Ipo siku ntapata

Nasubiri Bado Video

  • Song: Nasubiri Bado
  • Artist(s): Peter Blessing


Share: