1 Petro Mlango 4 1st Peter

1 Petro 4:1 1stPeter 4:1

Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi.

1 Petro 4:2 1stPeter 4:2

Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.

1 Petro 4:3 1stPeter 4:3

Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;

1 Petro 4:4 1stPeter 4:4

mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana.

1 Petro 4:5 1stPeter 4:5

Nao watatoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa.

1 Petro 4:6 1stPeter 4:6

Maana kwa ajili hiyo hata hao waliokufa walihubiriwa Injili, ili kwamba wahukumiwe katika mwili kama wahukumiwavyo wanadamu; bali wawe hai katika roho kama Mungu alivyo hai.

1 Petro 4:7 1stPeter 4:7

Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iweni na akili, mkeshe katika sala.

1 Petro 4:8 1stPeter 4:8

Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi.

1 Petro 4:9 1stPeter 4:9

Mkaribishane ninyi kwa ninyi, pasipo kunung'unika;

1 Petro 4:10 1stPeter 4:10

kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu.

1 Petro 4:11 1stPeter 4:11

Mtu akisema, na aseme kama mausia ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina.

1 Petro 4:12 1stPeter 4:12

Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.

1 Petro 4:13 1stPeter 4:13

Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.

1 Petro 4:14 1stPeter 4:14

Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia.

1 Petro 4:15 1stPeter 4:15

Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine.

1 Petro 4:16 1stPeter 4:16

Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.

1 Petro 4:17 1stPeter 4:17

Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya Mungu; na ikianza kwetu sisi, mwisho wao wasioitii injili ya Mungu utakuwaje?

1 Petro 4:18 1stPeter 4:18

Na mwenye haki akiokoka kwa shida, yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi ataonekana wapi?

1 Petro 4:19 1stPeter 4:19

Basi wao wateswao kwa mapenzi ya Mungu na wamwekee amana roho zao, katika kutenda mema, kama kwa Muumba mwaminifu.