Waefeso Mlango 1 Ephesians

Waefeso 1:1 Ephesians 1:1

Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu; kwa watakatifu walioko [Efeso] wanaomwamini Kristo Yesu.

Waefeso 1:2 Ephesians 1:2

Neema na iwe kwenu na amani zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.

Waefeso 1:3 Ephesians 1:3

Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;

Waefeso 1:4 Ephesians 1:4

kama vile alivyotuchagua katika yeye kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili tuwe watakatifu, watu wasio na hatia mbele zake katika pendo.

Waefeso 1:5 Ephesians 1:5

Kwa kuwa alitangulia kutuchagua, ili tufanywe wanawe kwa njia ya Yesu Kristo, sawasawa na uradhi wa mapenzi yake.

Waefeso 1:6 Ephesians 1:6

Na usifiwe utukufu wa neema yake, ambayo ametuneemesha katika huyo Mpendwa.

Waefeso 1:7 Ephesians 1:7

Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.

Waefeso 1:8 Ephesians 1:8

Naye alituzidishia hiyo katika hekima yote na ujuzi;

Waefeso 1:9 Ephesians 1:9

akiisha kutujulisha siri ya mapenzi yake, sawasawa na uradhi wake, alioukusudia katika yeye huyo.

Waefeso 1:10 Ephesians 1:10

Yaani, kuleta madaraka ya wakati mkamilifu atavijumlisha vitu vyote katika Kristo, vitu vya mbinguni na vitu vya duniani pia. Naam, katika yeye huyo;

Waefeso 1:11 Ephesians 1:11

na ndani yake sisi nasi tulifanywa urithi, huku tukichaguliwa tangu awali sawasawa na kusudi lake yeye, ambaye hufanya mambo yote kwa shauri la mapenzi yake.

Waefeso 1:12 Ephesians 1:12

Nasi katika huyo tupate kuwa sifa ya utukufu wake, sisi tuliotangulia kumwekea Kristo tumaini letu.

Waefeso 1:13 Ephesians 1:13

Nanyi pia katika huyo mmekwisha kulisikia neno la kweli, habari njema za wokovu wenu; tena mmekwisha kumwamini yeye, na kutiwa muhuri na Roho yule wa ahadi aliye Mtakatifu.

Waefeso 1:14 Ephesians 1:14

Ndiye aliye arabuni ya urithi wetu, ili kuleta ukombozi wa milki yake, kuwa sifa ya utukufu wake.

Waefeso 1:15 Ephesians 1:15

Kwa sababu hiyo mimi nami, tangu nilipopata habari za imani yenu katika Bwana Yesu, na pendo lenu kwa watakatifu wote,

Waefeso 1:16 Ephesians 1:16

siachi kutoa shukrani kwa ajili yenu; nikiwakumbuka katika sala zangu,

Waefeso 1:17 Ephesians 1:17

Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye;

Waefeso 1:18 Ephesians 1:18

macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo;

Waefeso 1:19 Ephesians 1:19

na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake;

Waefeso 1:20 Ephesians 1:20

aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho;

Waefeso 1:21 Ephesians 1:21

juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;

Waefeso 1:22 Ephesians 1:22

akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo

Waefeso 1:23 Ephesians 1:23

ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.