Waebrania Mlango 6 Hebrews

Waebrania 6:1 Hebrews 6:1

Kwa sababu hiyo, tukiacha kuyanena mafundisho ya kwanza ya Kristo, tukaze mwendo ili tuufikilie utimilifu; tusiweke msingi tena wa kuzitubia kazi zisizo na uhai, na wa kuwa na imani kwa Mungu,

Waebrania 6:2 Hebrews 6:2

na wa mafundisho ya mabatizo, na kuwekea mikono, na kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele.

Waebrania 6:3 Hebrews 6:3

Na hayo tutafanya Mungu akitujalia.

Waebrania 6:4 Hebrews 6:4

Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,

Waebrania 6:5 Hebrews 6:5

na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,

Waebrania 6:6 Hebrews 6:6

wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

Waebrania 6:7 Hebrews 6:7

Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu;

Waebrania 6:8 Hebrews 6:8

bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.

Waebrania 6:9 Hebrews 6:9

Lakini, wapenzi, ijapokuwa twanena hayo, katika habari zenu tumesadiki mambo yaliyo mazuri zaidi, na yaliyo na wokovu.

Waebrania 6:10 Hebrews 6:10

Maana Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu, na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake, kwa kuwa mmewahudumia watakatifu, na hata hivi sasa mngali mkiwahudumia.

Waebrania 6:11 Hebrews 6:11

Nasi twataka sana kila mmoja wenu aidhihirishe bidii ile ile, kwa utimilifu wa matumaini hata mwisho;

Waebrania 6:12 Hebrews 6:12

ili msiwe wavivu, bali mkawe wafuasi wa hao wazirithio ahadi kwa imani na uvumilivu.

Waebrania 6:13 Hebrews 6:13

Kwa maana Mungu, alipompa Ibrahimu ahadi, kwa sababu alikuwa hana mkubwa kuliko yeye mwenyewe wa kumwapa, aliapa kwa nafsi yake,

Waebrania 6:14 Hebrews 6:14

akisema, Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza.

Waebrania 6:15 Hebrews 6:15

Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi.

Waebrania 6:16 Hebrews 6:16

Maana wanadamu huapa kwa yeye aliye mkuu kuliko wao; na kwao ukomo wa mashindano yote ya maneno ni kiapo, kwa kuyathibitisha.

Waebrania 6:17 Hebrews 6:17

Katika neno hilo Mungu, akitaka kuwaonyesha zaidi sana warithio ile ahadi, jinsi mashauri yake yasivyoweza kubadilika, alitia kiapo katikati;

Waebrania 6:18 Hebrews 6:18

ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo, tupate faraja iliyo imara, sisi tuliokimbilia kuyashika matumaini yale yawekwayo mbele yetu;

Waebrania 6:19 Hebrews 6:19

tuliyo nayo kama nanga ya roho, yenye salama, yenye nguvu, yaingiayo hata mle mlimo ndani ya pazia,

Waebrania 6:20 Hebrews 6:20

alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu, amekuwa kuhani mkuu hata milele kwa mfano wa Melkizedeki.