Tito Mlango 2 Titus

Tito 2:1 Titus 2:1

Lakini wewe nena mambo yapasayo mafundisho yenye uzima;

Tito 2:2 Titus 2:2

ya kwamba wazee wawe wenye kiasi, wastahivu, wenye busara, wazima katika imani na katika upendo na katika saburi.

Tito 2:3 Titus 2:3

Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wafundishao mema;

Tito 2:4 Titus 2:4

ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao;

Tito 2:5 Titus 2:5

na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe.

Tito 2:6 Titus 2:6

Vivyo hivyo na vijana waume uwaonye kuwa na kiasi;

Tito 2:7 Titus 2:7

katika mambo yote ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika mafundisho yako ukionyesha usahihi na ustahivu,

Tito 2:8 Titus 2:8

na maneno yenye uzima yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga atahayarike, kwa kuwa hana neno baya la kunena juu yetu.

Tito 2:9 Titus 2:9

Watumwa na wawatii bwana zao, wakiwapendeza katika mambo yote; wasiwe wenye kujibu,

Tito 2:10 Titus 2:10

wasiwe waibaji; bali wauonyeshe uaminifu mwema wote, ili wayapambe mafundisho ya Mwokozi wetu Mungu katika mambo yote.

Tito 2:11 Titus 2:11

Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa;

Tito 2:12 Titus 2:12

nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa;

Tito 2:13 Titus 2:13

tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu;

Tito 2:14 Titus 2:14

ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema.

Tito 2:15 Titus 2:15

Nena maneno hayo, onya na kukaripia kwa mamlaka yote; asikudharau mtu awaye yote.