Beda Andrew - Mbali Sana

Chorus / Description : Ulikonitoa ni mbali sana
Ni kweli umenikomboa nashukuru sana
Ulikonitoa ni mbali sana
Ukanikomboa na zile laana

Mbali sana, mbali sana
Mbali sana nashukuru Bwana

Mbali Sana Lyrics

Na na na na... 
Nalikuwa sijiwezi unyonge ulinilemea 
Sikuwa na tumaini ya mbele kuendelea 
Imani ilififia sikuona kabisa
Kama moja ya nyenzo iliyotikisika aah 
Nalikosa tabasamu usoni 
Tegemeo sikuona maishani 
Nikashindwa endelea mbele 
Hali iliyofanya nikwame kule 

Ulikonitoa ni mbali sana 
Ni kweli umenikomboa nashukuru sana 
Ulikonitoa ni mbali sana 
Ukanikomboa na zile laana 

Mbali sana, mbali sana 
Mbali sana nashukuru Bwana 

Uliona haiko shwari mimi kupotea njia 
Sijui namna gani uliwaza ukanihurumia 
Nalifanya nia jangwa mvua kutonyeshe 
Nami mche mbichi maji yalinikaukia 
Shida mateso sina tena, yamewekwa nyuma 
Mimi wa Yesu mwingine sina 
Wa kurudisha nyuma 
Wakati wa kuokolewa umekubalika 
Kwa haki na ushupavu wake ukatibitika 

Ulikonitoa ni mbali sana 
Ni kweli umenikomboa nashukuru sana 
Ulikonitoa ni mbali sana 
Ukanikomboa na zile laana 

Mbali sana, mbali sana 
Mbali sana nashukuru Bwana 

oooh oh oh oooh 
...

Mbali Sana Video

  • Song: Mbali Sana
  • Artist(s): Beda Andrew


Share: