Chorus / Description :
Ameshinda Yesu kifo na kaburi
Ameshinda Yesu mfalme wa amani
Wakamshinda kwa neno la ushuhuda
Wakamshinda kwa damu ya mwanakondoo
Kulikuwa na vita mbinguni
Malaika wa Mungu
Walipigana na yule joka
Adui wa imani
Wakamshinda kwa neno la ushuhuda
Wakamshinda kwa damu ya mwanakondoo
Ameshinda Yesu kifo na kaburi
Ameshinda Yesu mfalme wa amani
Halleluya Halleluya
Halleluya Halleluya
Tumeingia kwenye agano
Agano la milele
Tumewekewa muhuri kwa damu
Damu ya mwanakondoo
Upande wetu sisi ni washindi
Tumeshinda pamoja naye
Kwa kumuamini Yesu kaingia moyoni
Tutatawala pamoja naye
Ameshinda Yesu kifo na kaburi
Ameshinda Yesu mfalme wa amani
Halleluya Halleluya
Halleluya Halleluya
Alizidi enzi mamlaka
Kagongemelewa msalabani
*Akaziuia mkoko alipokuwa Goligotha
Adhabu Ya Mungu kwa wanadamu
Ilikuwa begani mwake
Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona
Ushindi tunao
Ameshinda Yesu kifo na kaburi
Ameshinda Yesu mfalme wa amani
Halleluya Halleluya
Halleluya Halleluya
Habari njema zienee
Mataifa yasikie
Mfalme wetu Yesu kristo
Ameshinda kifo na kaburi
Wivu wa Mungu umezidi
Alikumbuka agano lake
Uzao wa mwanamke
Utakuponda kichwa wewe joka
Yesu uzao wa mwanamke
Amemponda kichwa joka shetani
Tumeuona utukufu kama wa mwana pekee wa Mungu
Yaliyonenwa na manabii torati na waamuzi
Yametimia mikononi mwake
Yesu mwana wa Mungu
Ameshinda Yesu kifo na kaburi
Ameshinda Yesu mfalme wa amani