Lyrics Page

29 Baba yetu aliye Mbinguni - Anipenda Mwokozi Yesu

By Angela Chibalonza

1,232 views Jun 6, 2026 updated

Baba yetu aliye mbinguni, amenifurahisha yakini,
kuniambia mwake chuoni, ya kuwa nami Yesu pendoni.

Anipenda Mwokozi Yesu, anipenda, anipenda;
Anipenda Mwokozi Yesu, anipenda mimi.

Nimuachapo kutanga mbali, yeye yu vivyo, hupenda kweli,
hunirejeza kwake moyoni; kweli yu nami Yesu pendoni.

Anipenda! Nami nampenda; kwa wokovu alionitenda;
akanifia Msalabani, kwa kuwa nami Yesu pendoni.

Haya kujua yanipa raha; kumuamini kuna furaha;
Humfukuza mara shetani, kwona yu nami Yesu Pendoni.

Sifa ni nyingi asifiwazo, moja ni sana katika hizo,
wala siachi, hata Mbinguni, kwimba, "Yu nami Yesu pendoni".

Official Video

Save Your Favorites

Create a free account to save songs, build your personal library, and connect with the Zion community.

Create Free Account

Join the Zion Community

Create a free account to save your favorite lyrics, submit song suggestions, and connect with fellow worshippers.

No spam. Unsubscribe anytime.