Wamwendea Yesu kwa kusafiwa,
na kuoshwa kwa damu ya kondoo?
je neema yake atumwagia,
tumeoshwa kwa damu ya kondoo?
Kuoshwa, kwa damu,
itutakasayo ya kondoo;
ziwe safi nguo nyeupe mno;
umeoshwa kwa damu ya kondoo?
Wamwandama daima mkombozi,
na kuoshwa na damu ya kondoo?
yako kwa msulubiwa makazi,
umeoshwa kwa damu ya kondoo?
Kuoshwa, kwa damu,
itutakasayo ya kondoo;
ziwe safi nguo nyeupe mno;
umeoshwa kwa damu ya kondoo?
Atakapokuja Bwana -arusi,
Uwe safi kwa damu ya kondoo!
Yafae kwenda mbinguni mavazi,
Yafuliwe kwa damu ya kondoo.
Kuoshwa, kwa damu,
itutakasayo ya kondoo;
ziwe safi nguo nyeupe mno;
umeoshwa kwa damu ya kondoo?
Yatupwe yaliyo na takataka,
na uoshwe kwa damu ya kondoo.
Huoni kijito chatiririka,
na uoshwe kwa damu ya kondoo?
Kuoshwa, kwa damu,
itutakasayo ya kondoo;
ziwe safi nguo nyeupe mno;
umeoshwa kwa damu ya kondoo?
Wamwendea Yesu Kwa Kusafiwa na kuoshwa kwa damu ya Kondoo
Angela Chibalonza and Tutakizunguka Gospel Choir perform 'Wamwendea Yesu kwa Kusafiwa,' a Swahili hymn based on the classic 'Have You Been to Jesus for the Cleansing Power?' The song asks listeners if they have been washed in the blood of the Lamb, emphasizing spiritual purification and readiness for Christ's return. It calls for white robes made clean through Jesus' sacrifice, urging believers to forsake sin and be made holy. The lyrics reflect a traditional gospel message of salvation and sanctification, drawing on imagery of cleansing and the wedding feast of the Lamb.