Chorus / Description :
Huongoza hunishika, kwa mkono wa hakika
Nitaandamana naye Kristo aniongozaye
Huniongoza Mwokozi,
ndipo nami hufurahi
Niendapo pote napo,
ataniongoza papo
Huongoza hunishika, kwa mkono wa hakika
Nitaandamana naye Kristo aniongozaye
Pengine ni mashakani,
nami pengine rahani
Ni radhi ijayo yote,
yupo nami siku zote
Huongoza hunishika, kwa mkono wa hakika
Nitaandamana naye Kristo aniongozaye
Mkono akinishika,
kamwe sitanung?unika
Atachoniletea,
ni tayari kupokea
Huongoza, hunishika kwa mkono wa hakika
Nitaandamana naye Kristu aniongozaye
Nikiishika kazi chini,
nitakwenda huko mbinguni
Nako nitamtukuza,
Kristo aliyeniongoza
Huongoza hunishika, kwa mkono wa hakika
Nitaandamana naye Kristo aniongozaye
Nitaandamana naye kristo aniongozayeÂ
Nitaandamana naye kristo aniongozaye
Nitaandamana naye kristo aniongozaye