Pst. Emmanuel Ushindi - Uheshimiwe Baba - Nikupe Mungu Nini

Chorus / Description : Nikupe Mungu nini?
Nifanye kazi gani?
Wala niseme Neno Gani
Nipate Kimbali Mbele Yako
Uheshimiwe Baba, Uheshimiwe Baba
Uheshimiwe Eeh, uheshimiwe Baba
Uabudiwe Baba, uabudiwe Baba
Uabudiwe Baba eeh
Unanilewesha Bwana, unanilewesha sana
Unanilewesha eeh, Unanilewesha Bwana

Uheshimiwe Baba - Nikupe Mungu Nini Lyrics

Nikupe Mungu nini?
Nifanye kazi gani?
Wala niseme Neno gani
Nipate Kimbali Mbele Yako
Unitaje Kati Ya Wale Watatu
Unao Jivunia, Washikao Mbedera Yako
Ili Wakuheshimishe, 
Juu Mimi Nimegundua Siri,
Yesu Uko Mali Yangu,
Uko Nguvu Zangu, Na Heshima Yangu
Shuhuda Yako Ni Urithi Wangu
Tena Changamko Ya Moyo Wangu
Ulimwengu muniruhusu Eeeh 
Uhechimiwe Baba

Uheshimiwe Baba, Uheshimiwe Baba 
Uheshimiwe Eeh, uheshimiwe Baba

Heshima yako Baba inayo wivu sana 
Kama vile mwanaume aweka wivu ju ya mke wake 
Ilimshtua Samweli kuona Isreali inaomba mfalme 
Ijapo wana Mungu wa Kweli, Samweli akaogopa 
Alimtuma Nebukadineza, anasukumwa ndani ya mwitu 
Akale majani kama mnyama, sababu alikusahau 
Mfalme moja akalewa, kamata vyombo vya hekalu vitakatidu 
Akavinyeshweya makahaba, kumbe Mungu una wivu 
Message ikatoka mbinguni, ikaandika 
"mene mene tekel upharsin", Ufalme wako umepimwa 
Ona unapewa wengine 
Hasira zako zilitumia Herodi, alipokamata Petro 
akataka mchinga akamuue, akatumia tena kukamata pepo 
Hapo malaika akatoka mbinguni... 
Herodi alipoamka, akakute Petro amekwenda 
Asikari wakashindwa, akasema muandae mkutano 
Aliposema maneno kama mfalme, watu wakapiga mkono 
Wakasema Herode si wewe, lakini sauti yako ni kama Munguu 
Mungu mbinguni akasirika, Herodi tumbo zikatoboka akafa hivo...
Uabudiwe Baba, uabudiwe Baba 
Uabudiwe Baba eeh

Uheshimiwe Baba, Uheshimiwe Baba 
Uheshimiwe Eeh, uheshimiwe Baba 

Najijua kama kabinti, mwanaume hawezi kuniponyoka 
Mabembelenzi ya delila ilimsukuma Samsoni kutoa siri 
Na mimi sitatoka bila Yesu siendi fasi kama siko nawe 
Hata nikilala kitandani nisipokuona Yesu mpaka nitaamuka 
Nitawaambia walinzi wa mji, nitafutieni Yesu mpaka nimshike 
Ahadi zako zanichumbia, maneno yako lasukuma nikupende 
Uko mtamu kwangu unaninogea sana, niende wapi bila wewe? 
Ona mi nalewa sasa, nalewa furaha yako Baba 
Eeeh haleluya ooh haleluya 

Unanilewesha Bwana, unanilewesha sana 
Unanilewesha eeh, Unanilewesha Bwana 

Unanilewesha Bwana, unanilewesha sana 
Unanilewesha eeh, Unanilewesha Bwana

Uheshimiwe Baba - Nikupe Mungu Nini Video

  • Song: Uheshimiwe Baba - Nikupe Mungu Nini
  • Artist(s): Pst. Emmanuel Ushindi


Share: