Reuben Kigame - Usifadhaike

Chorus / Description : Unalia nini ndugu yangu wee
Kodi ya nyumba na kazi huna
Na watoto wako hawana karo
Hata uko shuleni wamefukuzwa
Oh ooh ooh anasema wewe ni wa maana sana kuliko vyote
Na tena umeandikwa kwa kiganja chake oh ooh usifadahike

Usifadhaike Lyrics

Usifadhaike ndugu yangu wee 
Ule nini unywe nini kila siku 
Ama uvae nini dada yangu wee 
Baba wako wa mbinguni ashugulika 
Asema u wathamani kuliko wale ndege 
wasiopanda wa kuvuna aah 
Na tena u wathamani kuliko na maua ya kondeni 

Usifadhaike mteule we 
Majaribu na maonjo kila upande 
Ukidharauliwa na kusemwa semwa eh 
Hata imani yako yadidimia 
Asema anafahamu wewe una nguvu ndogo 
Lakini umesimama 
Na tena yuko na wewe hadi mwisho wa dahari 
Kwa hivyo usifadhaike 

Usifadhaike oh mjane wee 
Uliyeishi naye amekuacha 
Na watoto wako sasa ni yatima eeh 
Marafiki na jamii wametoroka 
Asema anasikia sauti ya mjane Oh ooh amwitapo 
Na tena yeye ni Baba wa yatima wote usifadhaike 

Unalia nini ndugu yangu wee 
Kodi ya nyumba na kazi huna 
Na watoto wako hawana karo 
Hata uko shuleni wamefukuzwa 
Oh ooh ooh anasema wewe ni wa maana sana kuliko vyote 
Na tena umeandikwa kwa kiganja chake oh ooh usifadahike 

Usijaribu kufadhaika (usifadhaike) 
Yeye ana hesabu ya nywele zako (usifadhaike) 
Ukifadhaika utakonda (usifadhaike) 
Kaka yangu wee (usifadhaike) 
Yeye anajua kesho (usifadhaike) 
Usifadhaike mummy (usifadhaike) 
Mtoto usifadhaike (usifadhaike) 
Hizi ni ahadi zake (usifadhaike)

Usifadhaike Video

  • Song: Usifadhaike
  • Artist(s): Reuben Kigame


Share: