2 Wathesalonike Mlango 1 2dThessalonians
2 Wathesalonike 1:1 2dThessalonians 1:1
Paulo, na Silwano, na Timotheo, kwa kanisa la Wathesalonike, lililo katika Mungu Baba yetu, na Bwana Yesu Kristo.
2 Wathesalonike 1:2 2dThessalonians 1:2
Neema na iwe kwenu na amani zitokazo kwa Mungu Baba, na kwa Bwana Yesu Kristo.
2 Wathesalonike 1:3 2dThessalonians 1:3
Ndugu, imetupasa kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, kama ilivyo wajibu, kwa kuwa imani yenu inazidi sana, na upendo wa kila mtu kwenu kwa mwenzake umekuwa mwingi.
2 Wathesalonike 1:4 2dThessalonians 1:4
Hata na sisi wenyewe twaona fahari juu yenu katika makanisa ya Mungu kwa ajili ya saburi yenu, na imani mliyo nayo katika adha zenu zote na dhiki mnazostahimili.
2 Wathesalonike 1:5 2dThessalonians 1:5
Ndiyo ishara hasa ya hukumu iliyo haki ya Mungu, ili mhesabiwe kuwa mwastahili kuuingia ufalme wa Mungu, ambao kwa ajili yake mnateswa.
2 Wathesalonike 1:6 2dThessalonians 1:6
Kwa kuwa ni haki mbele za Mungu kuwalipa mateso wale wawatesao ninyi;
2 Wathesalonike 1:7 2dThessalonians 1:7
na kuwalipa ninyi mteswao raha pamoja na sisi; wakati wa kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake
2 Wathesalonike 1:8 2dThessalonians 1:8
katika mwali wa moto; huku akiwalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu;
2 Wathesalonike 1:9 2dThessalonians 1:9
watakaoadhibiwa kwa maangamizi ya milele, kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa nguvu zake;
2 Wathesalonike 1:10 2dThessalonians 1:10
yeye atakapokuja ili kutukuzwa katika watakatifu wake, na kustaajabiwa katika wote waliosadiki katika siku ile, (kwa sababu ushuhuda wetu ulisadikiwa kwenu).
2 Wathesalonike 1:11 2dThessalonians 1:11
Kwa hiyo twawaombea ninyi sikuzote, ili Mungu wetu awahesabu kuwa mmekustahili kuitwa kwenu, akatimiza kila haja ya wema na kila kazi ya imani kwa nguvu;
2 Wathesalonike 1:12 2dThessalonians 1:12
jina la Bwana wetu Yesu litukuzwe ndani yenu, nanyi ndani yake, kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.