2 Wathesalonike Mlango 2 2dThessalonians
2 Wathesalonike 2:1 2dThessalonians 2:1
Basi, ndugu, tunakusihini, kwa habari ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, na kukusanyika kwetu mbele zake,
2 Wathesalonike 2:2 2dThessalonians 2:2
kwamba msifadhaishwe upesi hata kuiacha nia yenu, wala msisitushwe, kwa roho, wala kwa neno, wala kwa waraka unaodhaniwa kuwa ni wetu, kana kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwapo.
2 Wathesalonike 2:3 2dThessalonians 2:3
Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu;
2 Wathesalonike 2:4 2dThessalonians 2:4
yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.
2 Wathesalonike 2:5 2dThessalonians 2:5
Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?
2 Wathesalonike 2:6 2dThessalonians 2:6
Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.
2 Wathesalonike 2:7 2dThessalonians 2:7
Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.
2 Wathesalonike 2:8 2dThessalonians 2:8
Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake;
2 Wathesalonike 2:9 2dThessalonians 2:9
yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo;
2 Wathesalonike 2:10 2dThessalonians 2:10
na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.
2 Wathesalonike 2:11 2dThessalonians 2:11
Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo;
2 Wathesalonike 2:12 2dThessalonians 2:12
ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu.
2 Wathesalonike 2:13 2dThessalonians 2:13
Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, ndugu mliopendwa na Bwana, kwa kuwa Mungu amewachagua tangu mwanzo mpate wokovu, katika kutakaswa na Roho, na kuiamini kweli;
2 Wathesalonike 2:14 2dThessalonians 2:14
aliyowaitia ninyi kwa injili yetu, ili kuupata utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
2 Wathesalonike 2:15 2dThessalonians 2:15
Basi, ndugu, simameni imara, mkayashike mapokeo mliyofundishwa, ama kwa maneno, ama kwa waraka wetu.
2 Wathesalonike 2:16 2dThessalonians 2:16
Na Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe, na Mungu Baba yetu, aliyetupenda akatupa faraja ya milele na tumaini jema, katika neema,
2 Wathesalonike 2:17 2dThessalonians 2:17
awafariji mioyo yenu, na kuwafanya imara katika kila neno na tendo jema.