2 Wathesalonike Mlango 3 2dThessalonians
2 Wathesalonike 3:1 2dThessalonians 3:1
Hatimaye, ndugu, tuombeeni, neno la Bwana liendelee, na kutukuzwa vile vile kama ilivyo kwenu;
2 Wathesalonike 3:2 2dThessalonians 3:2
tukaokolewe na watu wasio haki, wabaya; maana si wote walio na imani.
2 Wathesalonike 3:3 2dThessalonians 3:3
Lakini Bwana ni mwaminifu, atakayewafanya imara na kuwalinda na yule mwovu.
2 Wathesalonike 3:4 2dThessalonians 3:4
Nasi tumemtumaini Bwana kwa mambo yenu, kwamba mnayafanya tulivyowaagiza, tena kwamba mtayafanya.
2 Wathesalonike 3:5 2dThessalonians 3:5
Bwana awaongoze mioyo yenu mkapate pendo la Mungu, na saburi ya Kristo.
2 Wathesalonike 3:6 2dThessalonians 3:6
Ndugu, twawaagiza katika jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni nafsi zenu na kila ndugu aendaye bila utaratibu, wala si kwa kufuata mapokeo mliyoyapokea kwetu.
2 Wathesalonike 3:7 2dThessalonians 3:7
Mwajua wenyewe jinsi iwapasavyo kutufuata; kwa sababu hatukuenda bila utaratibu kwenu;
2 Wathesalonike 3:8 2dThessalonians 3:8
wala hatukula chakula kwa mtu ye yote bure; bali kwa taabu na masumbufu, usiku na mchana tulitenda kazi, ili tusimlemee mtu wa kwenu awaye yote.
2 Wathesalonike 3:9 2dThessalonians 3:9
Si kwamba hatuna amri, lakini makusudi tufanye nafsi zetu kuwa kielelezo kwenu, mtufuate.
2 Wathesalonike 3:10 2dThessalonians 3:10
Kwa kuwa hata wakati ule tulipokuwapo kwenu tuliwaagiza neno hili, kwamba ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula.
2 Wathesalonike 3:11 2dThessalonians 3:11
Maana twasikia kwamba wako watu kwenu waendao bila utaratibu, hawana shughuli zao wenyewe, lakini wanajishughulisha na mambo ya wengine.
2 Wathesalonike 3:12 2dThessalonians 3:12
Basi twawaagiza hao, na kuwaonya katika Bwana Yesu Kristo, watende kazi kwa utulivu na kula chakula chao wenyewe.
2 Wathesalonike 3:13 2dThessalonians 3:13
Lakini ninyi, ndugu, msikate tamaa katika kutenda mema.
2 Wathesalonike 3:14 2dThessalonians 3:14
Na ikiwa mtu awaye yote halishiki neno letu la waraka huu, jihadharini na mtu huyo, wala msizungumze naye, apate kutahayari;
2 Wathesalonike 3:15 2dThessalonians 3:15
lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.
2 Wathesalonike 3:16 2dThessalonians 3:16
Sasa, Bwana wa amani mwenyewe na awape amani daima kwa njia zote. Bwana awe pamoja nanyi nyote.
2 Wathesalonike 3:17 2dThessalonians 3:17
Salamu zangu mimi Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndiyo alama katika kila waraka, ndio mwandiko wangu.
2 Wathesalonike 3:18 2dThessalonians 3:18
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi nyote.