2 Timotheo Mlango 4 2nd Timothy

2 Timotheo 4:1 2ndTimothy 4:1

Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu walio hai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake;

2 Timotheo 4:2 2ndTimothy 4:2

lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho.

2 Timotheo 4:3 2ndTimothy 4:3

Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masikio ya utafiti;

2 Timotheo 4:4 2ndTimothy 4:4

nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo.

2 Timotheo 4:5 2ndTimothy 4:5

Bali wewe, uwe na kiasi katika mambo yote, vumilia mabaya, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiliza huduma yako.

2 Timotheo 4:6 2ndTimothy 4:6

Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika.

2 Timotheo 4:7 2ndTimothy 4:7

Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;

2 Timotheo 4:8 2ndTimothy 4:8

baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.

2 Timotheo 4:9 2ndTimothy 4:9

Jitahidi kuja kwangu upesi.

2 Timotheo 4:10 2ndTimothy 4:10

Maana Dema aliniacha, akiupenda ulimwengu huu wa sasa, akasafiri kwenda Thesalonike; Kreske amekwenda Galatia; Tito amekwenda Dalmatia.

2 Timotheo 4:11 2ndTimothy 4:11

Luka peke yake yupo hapa pamoja nami. Umtwae Marko, umlete pamoja nawe, maana anifaa kwa utumishi.

2 Timotheo 4:12 2ndTimothy 4:12

Lakini Tikiko nalimpeleka Efeso.

2 Timotheo 4:13 2ndTimothy 4:13

Lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa, ujapo ulilete, na vile vitabu, hasa vile vya ngozi.

2 Timotheo 4:14 2ndTimothy 4:14

Iskanda, mfua shaba, alionyesha ubaya mwingi kwangu; Bwana atamlipa sawasawa na matendo yake.

2 Timotheo 4:15 2ndTimothy 4:15

Nawe ujihadhari na huyo, kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu.

2 Timotheo 4:16 2ndTimothy 4:16

Katika jawabu langu la kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu, bali wote waliniacha; naomba wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo.

2 Timotheo 4:17 2ndTimothy 4:17

Lakini Bwana alisimama pamoja nami akanitia nguvu, ili kwa kazi yangu ule ujumbe utangazwe kwa utimilifu, hata wasikie Mataifa yote; nami nikaokolewa katika kinywa cha simba.

2 Timotheo 4:18 2ndTimothy 4:18

Bwana ataniokoa na kila neno baya, na kunihifadhi hata nifike ufalme wake wa mbinguni. Utukufu una Yeye milele na milele. Amina.

2 Timotheo 4:19 2ndTimothy 4:19

Nisalimie Priska na Akila, na wale wa nyumbani mwa Onesiforo.

2 Timotheo 4:20 2ndTimothy 4:20

Erasto alikaa Korintho. Trofimo nalimwacha huko Mileto, hawezi.

2 Timotheo 4:21 2ndTimothy 4:21

Jitahidi kuja kabla ya wakati wa baridi. Eubulo akusalimu, na Pude, na Lino, na Klaudia, na ndugu wote pia.

2 Timotheo 4:22 2ndTimothy 4:22

Bwana na awe pamoja na roho yako. Neema na iwe pamoja nanyi.