2 Timotheo Mlango 3 2nd Timothy

2 Timotheo 3:1 2ndTimothy 3:1

Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.

2 Timotheo 3:2 2ndTimothy 3:2

Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,

2 Timotheo 3:3 2ndTimothy 3:3

wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema,

2 Timotheo 3:4 2ndTimothy 3:4

wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu;

2 Timotheo 3:5 2ndTimothy 3:5

wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.

2 Timotheo 3:6 2ndTimothy 3:6

Kwa maana katika hao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu, na kuchukua mateka wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi, waliochukuliwa na tamaa za namna nyingi;

2 Timotheo 3:7 2ndTimothy 3:7

wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.

2 Timotheo 3:8 2ndTimothy 3:8

Na kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Musa, vivyo hivyo na hawa wanapingana na ile kweli; ni watu walioharibika akili zao, wamekataliwa kwa mambo ya imani.

2 Timotheo 3:9 2ndTimothy 3:9

Lakini hawataendelea sana; maana upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama vile na upumbavu wa hao ulivyokuwa dhahiri.

2 Timotheo 3:10 2ndTimothy 3:10

Bali wewe umeyafuata mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na uvumilivu,

2 Timotheo 3:11 2ndTimothy 3:11

na upendo, na saburi; tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonio, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili, naye Bwana aliniokoa katika hayo yote.

2 Timotheo 3:12 2ndTimothy 3:12

Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa.

2 Timotheo 3:13 2ndTimothy 3:13

lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.

2 Timotheo 3:14 2ndTimothy 3:14

Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao;

2 Timotheo 3:15 2ndTimothy 3:15

na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu.

2 Timotheo 3:16 2ndTimothy 3:16

Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;

2 Timotheo 3:17 2ndTimothy 3:17

ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.