Maombolezo Mlango 5 Lamentations
Maombolezo 5:1 Lamentations 5:1
Ee Bwana, kumbuka yaliyotupata; Utazame na kuiona aibu yetu.
Maombolezo 5:2 Lamentations 5:2
Urithi wetu umegeuka kuwa mali ya wageni; Na nyumba zetu kuwa mali ya makafiri.
Maombolezo 5:3 Lamentations 5:3
Tumekuwa yatima waliofiwa na baba; Mama zetu wamekuwa kama wajane.
Maombolezo 5:4 Lamentations 5:4
Tumekunywa maji yetu kwa fedha; Kuni zetu twauziwa.
Maombolezo 5:5 Lamentations 5:5
Watufuatiao wa juu ya shingo zetu; Tumechoka tusipate raha yo yote.
Maombolezo 5:6 Lamentations 5:6
Tumewapa hao Wamisri mkono; Na Waashuri nao, ili tushibe chakula.
Maombolezo 5:7 Lamentations 5:7
Baba zetu walitenda dhambi hata hawako; Na sisi tumeyachukua maovu yao.
Maombolezo 5:8 Lamentations 5:8
Watumwa wanatutawala; Hakuna mtu wa kutuokoa na mikono yao.
Maombolezo 5:9 Lamentations 5:9
Twapata chakula kwa kujihatarisha nafsi zetu; Kwa sababu ya upanga wa nyikani.
Maombolezo 5:10 Lamentations 5:10
Ngozi yetu ni nyeusi kama tanuu; Kwa sababu ya hari ya njaa ituteketezayo.
Maombolezo 5:11 Lamentations 5:11
Huwatia jeuri wanawake katika Sayuni; Na mabikira katika miji ya Yuda.
Maombolezo 5:12 Lamentations 5:12
Wakuu hutungikwa kwa mikono yao; Nyuso za wazee hazipewi heshima.
Maombolezo 5:13 Lamentations 5:13
Vijana huyachukua mawe ya kusagia; Na watoto hujikwaa chini ya kuni.
Maombolezo 5:14 Lamentations 5:14
Wazee wameacha kwenda langoni; Na vijana kwenda ngomani.
Maombolezo 5:15 Lamentations 5:15
Furaha ya mioyo yetu imekoma; Machezo yetu yamegeuka maombolezo.
Maombolezo 5:16 Lamentations 5:16
Taji ya kichwa chetu imeanguka; Ole wetu! Kwa kuwa tumetenda dhambi.
Maombolezo 5:17 Lamentations 5:17
Kwa sababu hiyo mioyo yetu imezimia; Kwa ajili ya hayo macho yetu hayaoni vema.
Maombolezo 5:18 Lamentations 5:18
Kwa ajili ya mlima Sayuni ulio ukiwa, Mbweha hutembea juu yake.
Maombolezo 5:19 Lamentations 5:19
Wewe, Bwana, unadumu milele; Kiti chako cha enzi ni tangu kizazi hata kizazi.
Maombolezo 5:20 Lamentations 5:20
Mbona watusahau sikuzote; Na kutuacha muda huu mwingi?
Maombolezo 5:21 Lamentations 5:21
Ee Bwana, utugeuze kwako, nasi tutageuka; Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale.
Maombolezo 5:22 Lamentations 5:22
Isipokuwa wewe umetukataa kabisa; Nawe una hasira nyingi sana juu yetu.