Maombolezo Mlango 5 Lamentations

Maombolezo 5:1 Lamentations 5:1

Ee Bwana, kumbuka yaliyotupata; Utazame na kuiona aibu yetu.

Maombolezo 5:2 Lamentations 5:2

Urithi wetu umegeuka kuwa mali ya wageni; Na nyumba zetu kuwa mali ya makafiri.

Maombolezo 5:3 Lamentations 5:3

Tumekuwa yatima waliofiwa na baba; Mama zetu wamekuwa kama wajane.

Maombolezo 5:4 Lamentations 5:4

Tumekunywa maji yetu kwa fedha; Kuni zetu twauziwa.

Maombolezo 5:5 Lamentations 5:5

Watufuatiao wa juu ya shingo zetu; Tumechoka tusipate raha yo yote.

Maombolezo 5:6 Lamentations 5:6

Tumewapa hao Wamisri mkono; Na Waashuri nao, ili tushibe chakula.

Maombolezo 5:7 Lamentations 5:7

Baba zetu walitenda dhambi hata hawako; Na sisi tumeyachukua maovu yao.

Maombolezo 5:8 Lamentations 5:8

Watumwa wanatutawala; Hakuna mtu wa kutuokoa na mikono yao.

Maombolezo 5:9 Lamentations 5:9

Twapata chakula kwa kujihatarisha nafsi zetu; Kwa sababu ya upanga wa nyikani.

Maombolezo 5:10 Lamentations 5:10

Ngozi yetu ni nyeusi kama tanuu; Kwa sababu ya hari ya njaa ituteketezayo.

Maombolezo 5:11 Lamentations 5:11

Huwatia jeuri wanawake katika Sayuni; Na mabikira katika miji ya Yuda.

Maombolezo 5:12 Lamentations 5:12

Wakuu hutungikwa kwa mikono yao; Nyuso za wazee hazipewi heshima.

Maombolezo 5:13 Lamentations 5:13

Vijana huyachukua mawe ya kusagia; Na watoto hujikwaa chini ya kuni.

Maombolezo 5:14 Lamentations 5:14

Wazee wameacha kwenda langoni; Na vijana kwenda ngomani.

Maombolezo 5:15 Lamentations 5:15

Furaha ya mioyo yetu imekoma; Machezo yetu yamegeuka maombolezo.

Maombolezo 5:16 Lamentations 5:16

Taji ya kichwa chetu imeanguka; Ole wetu! Kwa kuwa tumetenda dhambi.

Maombolezo 5:17 Lamentations 5:17

Kwa sababu hiyo mioyo yetu imezimia; Kwa ajili ya hayo macho yetu hayaoni vema.

Maombolezo 5:18 Lamentations 5:18

Kwa ajili ya mlima Sayuni ulio ukiwa, Mbweha hutembea juu yake.

Maombolezo 5:19 Lamentations 5:19

Wewe, Bwana, unadumu milele; Kiti chako cha enzi ni tangu kizazi hata kizazi.

Maombolezo 5:20 Lamentations 5:20

Mbona watusahau sikuzote; Na kutuacha muda huu mwingi?

Maombolezo 5:21 Lamentations 5:21

Ee Bwana, utugeuze kwako, nasi tutageuka; Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale.

Maombolezo 5:22 Lamentations 5:22

Isipokuwa wewe umetukataa kabisa; Nawe una hasira nyingi sana juu yetu.