Maombolezo Mlango 3 Lamentations
Maombolezo 3:1 Lamentations 3:1
Mimi ni mtu aliyeona mateso Kwa fimbo ya ghadhabu yake.
Maombolezo 3:2 Lamentations 3:2
Ameniongoza na kuniendesha katika giza Wala si katika nuru.
Maombolezo 3:3 Lamentations 3:3
Hakika juu yangu augeuza mkono wake Mara kwa mara mchana wote.
Maombolezo 3:4 Lamentations 3:4
Amechakaza nyama yangu na ngozi yangu; Ameivunja mifupa yangu.
Maombolezo 3:5 Lamentations 3:5
Amejenga boma juu yangu, Na kunizungusha uchungu na uchovu.
Maombolezo 3:6 Lamentations 3:6
Amenikalisha penye giza, Kama watu waliokufa zamani.
Maombolezo 3:7 Lamentations 3:7
Amenizinga pande zote hata siwezi kutoka; Ameufanya mnyororo wangu mzito.
Maombolezo 3:8 Lamentations 3:8
Naam, nikilia na kuomba msaada, Huyapinga maombi yangu.
Maombolezo 3:9 Lamentations 3:9
Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa; Ameyapotosha mapito yangu.
Maombolezo 3:10 Lamentations 3:10
Alivyo kwangu ni kama dubu aoteaye, Kama simba aliye mafichoni.
Maombolezo 3:11 Lamentations 3:11
Amezigeuza njia zangu, na kunirarua-rarua; Amenifanya ukiwa.
Maombolezo 3:12 Lamentations 3:12
Ameupinda upinde wake, Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale.
Maombolezo 3:13 Lamentations 3:13
Amenichoma viuno Kwa mishale ya podo lake.
Maombolezo 3:14 Lamentations 3:14
Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote; Wimbo wao mchana kutwa.
Maombolezo 3:15 Lamentations 3:15
Amenijaza uchungu, Amenikinaisha kwa pakanga.
Maombolezo 3:16 Lamentations 3:16
Amenivunja meno kwa changarawe; Amenifunika majivu.
Maombolezo 3:17 Lamentations 3:17
Umeniweka nafsi yangu mbali na amani; Nikasahau kufanikiwa.
Maombolezo 3:18 Lamentations 3:18
Nikasema, Nguvu zangu zimepotea, Na tumaini langu kwa Bwana.
Maombolezo 3:19 Lamentations 3:19
Kumbuka mateso yangu, na msiba wangu, Pakanga na nyongo.
Maombolezo 3:20 Lamentations 3:20
Nafsi yangu ikali ikiyakumbuka hayo, Nayo imeinama ndani yangu.
Maombolezo 3:21 Lamentations 3:21
Najikumbusha neno hili, Kwa hiyo nina matumaini.
Maombolezo 3:22 Lamentations 3:22
Ni huruma za Bwana kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi.
Maombolezo 3:23 Lamentations 3:23
Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wako ni mkuu.
Maombolezo 3:24 Lamentations 3:24
Bwana ndiye fungu langu, husema nafsi yangu, Kwa hiyo nitamtumaini yeye.
Maombolezo 3:25 Lamentations 3:25
Bwana ni mwema kwa hao wamngojeao, Kwa hiyo nafsi imtafutayo.
Maombolezo 3:26 Lamentations 3:26
Ni vema mtu autarajie wokovu wa Bwana Na kumngojea kwa utulivu.
Maombolezo 3:27 Lamentations 3:27
Ni vema mwanadamu aichukue nira Wakati wa ujana wake.
Maombolezo 3:28 Lamentations 3:28
Na akae peke yake na kunyamaza kimya; Kwa sababu Bwana ameweka hayo juu yake.
Maombolezo 3:29 Lamentations 3:29
Na atie kinywa chake mavumbini; Ikiwa yamkini liko tumaini.
Maombolezo 3:30 Lamentations 3:30
Na amwelekezee yule ampigaye shavu lake; Ashibishwe mashutumu.
Maombolezo 3:31 Lamentations 3:31
Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele.
Maombolezo 3:32 Lamentations 3:32
Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.
Maombolezo 3:33 Lamentations 3:33
Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha.
Maombolezo 3:34 Lamentations 3:34
Kuwaseta chini kwa miguu Wafungwa wote wa duniani,
Maombolezo 3:35 Lamentations 3:35
Kuipotosha hukumu ya mtu Mbele zake Aliye juu,
Maombolezo 3:36 Lamentations 3:36
Na kumnyima mtu haki yake, Hayo Bwana hayaridhii kabisa.
Maombolezo 3:37 Lamentations 3:37
Ni nani asemaye neno nalo likafanyika, Ikiwa Bwana hakuliagiza?
Maombolezo 3:38 Lamentations 3:38
Je! Katika kinywa chake Aliye juu Hayatoki maovu na mema?
Maombolezo 3:39 Lamentations 3:39
Mbona anung'unika mwanadamu aliye hai Mtu akiadhibiwa kwa dhambi zake?
Maombolezo 3:40 Lamentations 3:40
Na tuchunguze njia zetu na kuzijaribu, Na kumrudia Bwana tena.
Maombolezo 3:41 Lamentations 3:41
Na tumwinulie Mungu aliye mbinguni Mioyo yetu na mikono.
Maombolezo 3:42 Lamentations 3:42
Sisi tumekosa na kuasi; Wewe hukusamehe.
Maombolezo 3:43 Lamentations 3:43
Umetufunika kwa hasira na kutufuatia; Umeua, wala hukuona huruma.
Maombolezo 3:44 Lamentations 3:44
Umejifunika nafsi yako kwa wingu, Maombi yetu yasipite.
Maombolezo 3:45 Lamentations 3:45
Umetufanya kuwa takataka, na vifusi Katikati ya mataifa.
Maombolezo 3:46 Lamentations 3:46
Juu yetu adui zetu wote Wametupanulia vinywa vyao.
Maombolezo 3:47 Lamentations 3:47
Hofu imetujilia na shimo, Ukiwa na uharibifu.
Maombolezo 3:48 Lamentations 3:48
Jicho langu lachuruzika mito ya maji Kwa ajili ya uvunjifu wa binti ya watu wangu.
Maombolezo 3:49 Lamentations 3:49
Jicho langu latoka machozi lisikome, Wala haliachi;
Maombolezo 3:50 Lamentations 3:50
Hata Bwana atakapoangalia Na kutazama toka mbinguni.
Maombolezo 3:51 Lamentations 3:51
Jicho langu lanitia huzuni nafsini mwangu, Kwa sababu ya binti zote za mji wangu.
Maombolezo 3:52 Lamentations 3:52
Walio adui zangu bila sababu Wameniwinda sana kama ndege;
Maombolezo 3:53 Lamentations 3:53
Wameukatilia mbali uhai wangu gerezani, Na kutupa jiwe juu yangu.
Maombolezo 3:54 Lamentations 3:54
Maji mengi yalipita juu ya kichwa changu, Nikasema, Nimekatiliwa mbali.
Maombolezo 3:55 Lamentations 3:55
Naliliitia jina lako, Bwana, kutoka lile shimo Liendalo chini kabisa.
Maombolezo 3:56 Lamentations 3:56
Ukaisikia sauti yangu; usifiche sikio lako Ili usisikie pumzi yangu, kwa kilio changu.
Maombolezo 3:57 Lamentations 3:57
Ulinikaribia siku ile nilipokulilia; Ukasema, Usiogope.
Maombolezo 3:58 Lamentations 3:58
Ee Bwana umenitetea mateto ya nafsi yangu; Umeukomboa uhai wangu.
Maombolezo 3:59 Lamentations 3:59
Umekuona kudhulumiwa kwangu, Ee Bwana; Unihukumie neno langu.
Maombolezo 3:60 Lamentations 3:60
Umekiona kisasi chao chote, Na mashauri yao yote juu yangu.
Maombolezo 3:61 Lamentations 3:61
Ee Bwana, umeyasikia matukano yao, Na mashauri yao yote juu yangu;
Maombolezo 3:62 Lamentations 3:62
Midomo yao walioinuka juu yangu Na maazimio yao juu yangu mchana kutwa.
Maombolezo 3:63 Lamentations 3:63
Uangalie kuketi kwao, na kuinuka kwao; Wimbo wao ndio mimi.
Maombolezo 3:64 Lamentations 3:64
Utawalipa malipo, Ee Bwana, Sawasawa na kazi ya mikono yao.
Maombolezo 3:65 Lamentations 3:65
Utawapa ushupavu wa moyo; Laana yako juu yao.
Maombolezo 3:66 Lamentations 3:66
Utawafuatia kwa hasira, na kuwaangamiza Wasiwe tena chini ya mbingu za Bwana.