Hesabu Mlango 17 Numbers

Hesabu 17:1 Numbers 17:1

Kisha Bwana akanena na Musa, akamwambia,

Hesabu 17:2 Numbers 17:2

Nena na wana wa Israeli, kisha upokee kwao fimbo, fimbo moja kwa ajili ya nyumba ya kila baba, katika wakuu wao wote, kama nyumba za baba zao zilivyo, fimbo kumi na mbili; kisha andika jina la kila mtu katika fimbo yake.

Hesabu 17:3 Numbers 17:3

Na katika fimbo ya Lawi utaliandika jina la Haruni; maana, itakuwa fimbo moja kwa kila kichwa cha nyumba za baba zao.

Hesabu 17:4 Numbers 17:4

Nawe utaziweka katika hema ya kukutania mbele ya huo ushahidi, hapo nikutanapo pamoja nanyi.

Hesabu 17:5 Numbers 17:5

Kisha itakuwa, mtu huyo nitakayemchagua, fimbo yake itachipuka; nami nitayakomesha kwangu manung'uniko ya wana wa Israeli, wanung'unikiayo juu yenu.

Hesabu 17:6 Numbers 17:6

Basi Musa akawaambia wana wa Israeli, ndipo wakuu wao wote wakampa fimbo, fimbo moja kwa kila mkuu, kama nyumba za baba zao zilivyokuwa, fimbo kumi na mbili; na fimbo ya Haruni ilikuwa kati ya fimbo zao.

Hesabu 17:7 Numbers 17:7

Kisha Musa akaziweka hizo fimbo mbele za Bwana katika hema ya kukutania.

Hesabu 17:8 Numbers 17:8

Ilikuwa siku ya pili yake, Musa akaingia ndani ya hema ya ushahidi; na tazama, ile fimbo ya Haruni iliyokuwa kwa nyumba ya Lawi ilikuwa imechipuka, imetoa michipukizi, na kuchanua maua; na kuzaa malozi mabivu.

Hesabu 17:9 Numbers 17:9

Kisha Musa akazileta nje hizo fimbo zote kutoka hapo mbele za Bwana na kuziweka mbele ya wana wa Israeli wote; nao wakaangalia, na kila mtu akaitwaa fimbo yake.

Hesabu 17:10 Numbers 17:10

Kisha Bwana akamwambia Musa, Irudishe fimbo ya Haruni mbele ya ushahidi, ili itunzwe iwe ishara juu ya hawa wana wa maasi; ili uyakomeshe manung'uniko yao waliyoninung'unikia, ili wasife.

Hesabu 17:11 Numbers 17:11

Basi Musa akafanya vivyo; kama Bwana alivyomwagiza, ndivyo alivyofanya.

Hesabu 17:12 Numbers 17:12

Kisha wana wa Israeli wakanena na Musa, na kumwambia, Angalia, sisi twafa, twaangamia, sote twaangamia.

Hesabu 17:13 Numbers 17:13

Kila mtu akaribiaye, aikaribiaye maskani ya Bwana, hufa; je! Tutakufa pia sote?