Hesabu Mlango 26 Numbers

Hesabu 26:1 Numbers 26:1

Ikawa baada ya hilo pigo, Bwana akanena na Musa na Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, na kuwaambia,

Hesabu 26:2 Numbers 26:2

Fanya jumla ya mkutano wote wa wana wa Israeli, tangu umri wa miaka ishirini, na zaidi, kwa nyumba za baba zao, hao wote katika Israeli wawezao kutoka kuenenda vitani.

Hesabu 26:3 Numbers 26:3

Kisha Musa na Eleazari kuhani wakanena nao katika nchi tambarare za Moabu karibu na mto wa Yordani, huko Yeriko, wakawaambia,

Hesabu 26:4 Numbers 26:4

Fanyeni jumla ya watu, tangu umri wa miaka ishirini, na zaidi; kama Bwana alivyomwagiza Musa na wana wa Israeli, hao waliotoka nchi ya Misri.

Hesabu 26:5 Numbers 26:5

Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli, wana wa Reubeni; wa Hanoki, jamaa ya Wahanoki; na wa Palu, jamaa ya Wapalu;

Hesabu 26:6 Numbers 26:6

na wa Hesroni, jamaa ya Wahesroni; na wa Karmi, jamaa ya Wakarmi.

Hesabu 26:7 Numbers 26:7

Hizi ndizo jamaa za Wareubeni; na hao waliohesabiwa kwao walikuwa arobaini na tatu elfu na mia saba na thelathini.

Hesabu 26:8 Numbers 26:8

Na wana wa Palu; Eliabu.

Hesabu 26:9 Numbers 26:9

Na wana wa Eliabu; Nemueli, na Dathani, na Abiramu. Hawa ndio Dathani na Abiramu waliochaguliwa na mkutano, ambao walishindana na Musa na Haruni katika mkutano wa Kora, hapo waliposhindana na Bwana;

Hesabu 26:10 Numbers 26:10

nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza pamoja na Kora, mkutano huo ulipokufa; wakati moto ulipowateketeza watu mia mbili na hamsini, nao wakawa ishara.

Hesabu 26:11 Numbers 26:11

Pamoja na hayo, hao wana wa Kora hawakufa.

Hesabu 26:12 Numbers 26:12

Na wana wa Simeoni kwa jamaa zao; wa Yemueli, jamaa ya Wayemueli; wa Yamini, jamaa ya Wayamini; na Yakini, jamaa ya Wayakini;

Hesabu 26:13 Numbers 26:13

wa Sohari, jamaa ya Wasohari; wa Shauli, jamaa ya Washauli.

Hesabu 26:14 Numbers 26:14

Hizi ndizo jamaa za Wasimeoni, watu ishirini na mbili elfu na mia mbili.

Hesabu 26:15 Numbers 26:15

Na wana wa Gadi kwa jamaa zao; wa Sifoni, jamaa ya Wasifoni; wa Hagi, jamaa ya Wahagi; wa Shuni, jamaa ya Washuni;

Hesabu 26:16 Numbers 26:16

wa Ezboni, jamaa ya Waezboni; wa Eri, jamaa ya Waeri;

Hesabu 26:17 Numbers 26:17

wa Arodi, jamaa ya Waarodi; wa Areli, jamaa ya Waareli.

Hesabu 26:18 Numbers 26:18

Hizi ndizo jamaa za wana wa Gadi kama waliohesabiwa kwao, arobaini elfu na mia tano.

Hesabu 26:19 Numbers 26:19

Na wana wa Yuda, Eri na Onani; na hao Eri na Onani wakafa katika nchi ya Kanaani.

Hesabu 26:20 Numbers 26:20

Na wana wa Yuda kwa jamaa zao; wa Shela, jamaa ya Washela; wa Peresi, jamaa ya Waperesi; wa Zera, jamaa ya Wazera.

Hesabu 26:21 Numbers 26:21

Na wana wa Peresi walikuwa; wa Hesroni, jamaa ya Wahesroni; wa Hamuli, jamaa ya Wahamuli.

Hesabu 26:22 Numbers 26:22

Hizi ndizo jamaa za Yuda kama waliohesabiwa kwao, sabini na sita elfu na mia tano.

Hesabu 26:23 Numbers 26:23

Na wana wa Isakari kwa jamaa zao; wa Tola, jamaa ya Watola; wa Puva, jamaa ya Wapuva;

Hesabu 26:24 Numbers 26:24

wa Yashubu, jamaa ya Wayashubu; wa Shimroni, jamaa ya Washimroni.

Hesabu 26:25 Numbers 26:25

Hizi ndizo jamaa za Isakari kama waliohesabiwa kwao, sitini na nne elfu na mia tatu.

Hesabu 26:26 Numbers 26:26

Na wana wa Zabuloni kwa jamaa zao; wa Seredi, jamaa ya Waseredi; wa Eloni, jamaa ya Waeloni; wa Yaleeli, jamaa ya Wayaleeli.

Hesabu 26:27 Numbers 26:27

Hizi ndizo jamaa za Wazabuloni kama waliohesabiwa kwao, sitini elfu na mia tano.

Hesabu 26:28 Numbers 26:28

Na wana wa Yusufu kwa jamaa zao; Manase na Efraimu.

Hesabu 26:29 Numbers 26:29

Wana wa Manase; wa Makiri, jamaa ya Wamakiri; na Makiri akamzaa Gileadi; wa Gileadi, jamaa ya Wagileadi.

Hesabu 26:30 Numbers 26:30

Hawa ndio wana wa Gileadi; wa Abiezeri, jamaa ya Waabiezeri; wa Heleki, jamaa ya Waheleki;

Hesabu 26:31 Numbers 26:31

na wa Asrieli, jamaa ya Waasrieli; na wa Shekemu, jamaa ya Washekemu;

Hesabu 26:32 Numbers 26:32

na wa Shemida, jamaa ya Washemida; na wa Heferi, jamaa ya Waheferi.

Hesabu 26:33 Numbers 26:33

Na Selofehadi mwana wa Heferi hakuwa na wana waume, isipokuwa wa kike; na majina ya hao binti za Selofehadi ni haya, Mala, na Noa, na Hogla, na Milka, na Tirsa.

Hesabu 26:34 Numbers 26:34

Hizi ndizo jamaa za Manase; na waliohesabiwa kwao walikuwa ni hamsini na mbili elfu na mia saba.

Hesabu 26:35 Numbers 26:35

Na wana wa Efraimu kwa jamaa zao; wa Shuthela, jamaa ya Washuthela; wa Beredi, jamaa ya Waberedi; wa Tahathi, jamaa ya Watahathi.

Hesabu 26:36 Numbers 26:36

Na wana wa Shuthela ni hawa; wa Erani, jamaa ya Waerani.

Hesabu 26:37 Numbers 26:37

Hizi ndizo jamaa za wana wa Efraimu kama waliohesabiwa kwao, thelathini na mbili elfu na mia tano. Hao ndio wana wa Yusufu kwa jamaa zao.

Hesabu 26:38 Numbers 26:38

Na wana wa Benyamini kwa jamaa zao; wa Bela, jamaa ya Wabela; na wa Ashbeli, jamaa ya Waashbeli; wa Ahiramu, jamaa ya Waahiramu;

Hesabu 26:39 Numbers 26:39

wa Shufamu, jamaa ya Washufamu; wa Hufamu, jamaa ya Wahufamu.

Hesabu 26:40 Numbers 26:40

Na wana wa Bela walikuwa Ardi na Naamani; wa Ardi, jamaa ya Waardi; wa Naamani, jamaa ya Wanaamani.

Hesabu 26:41 Numbers 26:41

Hao ndio wana wa Benyamini kwa jamaa zao; na waliohesabiwa kwao walikuwa arobaini na tano elfu na mia sita.

Hesabu 26:42 Numbers 26:42

Na wana wa Dani ni hawa kwa jamaa zao; wa Shuhamu, jamaa ya Washuhamu. Hizi ndizo jamaa za Dani kwa jamaa zao.

Hesabu 26:43 Numbers 26:43

Jamaa zote za Washuhamu, kama waliohesabiwa kwao, walikuwa sitini na nne elfu na mia nne.

Hesabu 26:44 Numbers 26:44

Na wana wa Asheri kwa jamaa zao; wa Imna, jamaa ya Waimna; wa Ishvi jamaa ya Waishvi; wa Beria, jamaa ya Waberia.

Hesabu 26:45 Numbers 26:45

Wa wana wa Beria; wa Heberi, jamaa ya Waheberi; wa Malkieli, jamaa ya Wamalkieli.

Hesabu 26:46 Numbers 26:46

Na jina la binti wa Asheri aliitwa Sera.

Hesabu 26:47 Numbers 26:47

Hizi ndizo jamaa za wana wa Asheri kama waliohesabiwa kwao, hamsini na tatu elfu na mia nne.

Hesabu 26:48 Numbers 26:48

Na wana wa Naftali kwa jamaa zake; wa Yaseeli, jamaa ya Wayaseeli; na wa Guni, jamaa ya Waguni;

Hesabu 26:49 Numbers 26:49

wa Yeseri, jamaa ya Wayeseri, wa Shilemu jamaa ya Washilemu.

Hesabu 26:50 Numbers 26:50

Hizi ndizo jamaa za Naftali kwa jamaa zao; na waliohesabiwa kwao walikuwa arobaini na tano elfu na mia nne.

Hesabu 26:51 Numbers 26:51

Hao ndio waliohesabiwa katika wana wa Israeli, mia sita na moja elfu, na mia saba na thelathini (601,730).

Hesabu 26:52 Numbers 26:52

Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

Hesabu 26:53 Numbers 26:53

Watu hawa watagawanyiwa nchi hiyo iwe urithi wao, vile vile kama hesabu ya majina yao ilivyo.

Hesabu 26:54 Numbers 26:54

Hao waliozidi hesabu yao utawapa urithi zaidi, na hao waliopunguka hesabu yao, utawapa urithi kama upungufu wao; kila mtu kama watu wake walivyohesabiwa, ndivyo atakavyopewa urithi wake.

Hesabu 26:55 Numbers 26:55

Lakini nchi itagawanywa kwa kura; kwa majina ya kabila za baba zao, ndivyo watakavyopata urithi.

Hesabu 26:56 Numbers 26:56

Kama kura itakavyokuwa, ndivyo urithi wao utakavyogawanywa kati yao, hao wengi na hao wachache.

Hesabu 26:57 Numbers 26:57

Na hao waliohesabiwa katika Walawi kwa jamaa zao ni hawa; wa Gershoni, jamaa ya Wagershoni; na wa Kohathi, jamaa ya Wakohathi; na wa Merari, jamaa ya Wamerari.

Hesabu 26:58 Numbers 26:58

Hizi ndizo jamaa za Lawi; jamaa ya Walibni, na jamaa ya Wahebroni, na jamaa ya Wamala, na jamaa ya Wamushi jamaa ya Wakora. Na Kohathi alimzaa Amramu.

Hesabu 26:59 Numbers 26:59

Na jina la mke wa Amramu aliitwa Yokebedi, binti wa Lawi, ambaye alizaliwa kwake Lawi huko Misri; na huyo Yokebedi akamzalia Amramu Haruni, na Musa, na Miriamu umbu lao.

Hesabu 26:60 Numbers 26:60

Tena kwake Haruni walizaliwa hawa, Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari.

Hesabu 26:61 Numbers 26:61

Tena Nadabu na Abihu wakafa, hapo waliposongeza moto wa kigeni mbele za Bwana.

Hesabu 26:62 Numbers 26:62

Na hao waliohesabiwa kwao walikuwa ishirini na tatu elfu, kila mwanamume tangu huyo aliyepata umri wa mwezi mmoja, na zaidi; kwa kuwa hawakuhesabiwa katika wana wa Israeli, kwa sababu hawakupewa urithi katika wana wa Israeli.

Hesabu 26:63 Numbers 26:63

Hao ndio waliohesabiwa na Musa na Eleazari kuhani; ambao waliwahesabu wana wa Israeli katika nchi tambarare za Moabu, karibu na Yordani, hapo Yeriko.

Hesabu 26:64 Numbers 26:64

Lakini katika watu hao hapakuwa na mtu hata mmoja wa wale waliohesabiwa na Musa na Haruni kuhani; waliowahesabu wana wa Israeli katika bara ya Sinai.

Hesabu 26:65 Numbers 26:65

Kwa kuwa Bwana alisema juu yao, Hapana budi watakufa nyikani. Napo hapakusalia mtu mmoja miongoni mwao, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni.