Christina Shusho - Akutendee Nini

Chorus / Description : Wataka akutendee nini?
Akutendee nini wewe,
Neno moja nalitaka kwa Bwana nalo ni hili
nikae nyumbani mwake siku zote za maisha yangu

Akutendee Nini Lyrics

Wataka akutendee nini?
Akutendee nini wewe,
Wataka akutende nini?
Akutende nini wewe,

"Neno moja nalitaka kwa Bwana nalo ni hili
nikae nyumbani mwake siku zote za maisha yangu"
Gala lake limejaa hakuna anayepunguza hata robo
Akutende nini wewe?
Wengine wataka kuwa raisi wa nchi
Wengine wataka ubunge
Akutendee nini wewe?
Mwengine ombi lake apate shamba
Huyu mume na huyu mke
Wataka akutendee nini wewe?
Mama huyu ombi lake apte mtoto
Mwengine apate elimu
Wataka akutende nini wewe?

Wataka akutendee nini?
Akutendee nini wewe,
Wataka akutende nini?
Akutende nini wewe,

Nakumbuka mgonjwa birikani
miaka thelathini na nane alikuwa hajiwezi yeye
Yesu akatetembelea birika lile
Akamwona mgonjwa yule
Mara akaanza sababu zake
"Malaika akifika akitubua maji
mimi huwa wa mwisho"
Yesu akasema neno moja
jitwike godoro lako na uende
Mara akawa mzima mzima

Wataka akutendee nini?
Akutendee nini wewe,
Wataka akutende nini?
Akutende nini wewe,

Akutendee Nini Video

  • Song: Akutendee Nini
  • Artist(s): Christina Shusho


Share: