Chorus / Description :
Naiona kesho kesho
Iliyopangwa na Baba
Naiona kesho kesho
Iliyopangwa na Mungu
Naiona kesho kesho
Iliyopangwa na Baba
Naiona kesho kesho
Iliyopangwa na Mungu .
Naiona kesho mimi kesho iliyopangwa na Baba
Kesho ya heshima aah iliyopangwa na Baba
kesho ya Neema iliyopangwa na Baba
Kesho yenye utukufu iliyopangwa na
Baba kesho ya kuinuliwa iliyopangwa na Baba
Kesho ya ushindi ii iliyopangwa na Mungu
Kesho yenye nguvu iliyopangwa na Baba .
Sitaki kuitazama leo yangu mwenzenu
Leo yangu ni shida mwenzenu
Leo yangu ni tabu mwenzenu
Leo machozi yanitoka aah mwenzenu
Leo nimekataliwa aah mwenzenu
Leo nimefukuzwa mapema mwenzenu
Leo wote waniacha aah mwenzenu
Leo machozi ni mengi hii mwenzenu .
Sitaki kuitazama Leo yangu kamwe
Sitaki kuitazama Leo yangu mimi
Leo yangu ninalia mwenzenu
Leo ninateseka aah mwenzenu
Leo mateso ni mengi hii mwenzenu .
Naiona kesho yangu mwenzenu
Naiona kesho yangu mwenzenu .
Japo vita yangu ni kubwa mwenzenu
Maadui wangu ni wengi mwenzenu
Japo mateso yangu ni magumu mwenzenu
Kuna neno amesema nami mwenzenu
Atapigana aah amesema
Atafanya mlango ooh amesema
Atanifanyia wepesi amesema .
Japo vita yangu kubwa mwenzenu
Japo adui ni wengi mwenzenu
Japo njia siioni mwenzenu
Atapigana mwenyewe amesema
Atafanya wepesi iiih amesema
Atanifanyia wepesi kwani amesema
Atanichunga salama amesema
Atafanya mlango ooh amesema
Atapigana na adui aah amesema .
Kasema niione kesho aliyoniwekea
Kasema niione kesho aliyoniwekea .
Kuna majira yalifika nikajua Mungu
Kuna majira yalifika nikamwelewa
Majira Yale yalikuwa magumu
Majira Yale yalikuwa magumu .
Kwa macho yangu nikaona akitenda
Akasema mwanangu nakupenda
Usiitazame Leo yako mwanangu
Ona mimi ni Mungu nikupendaye .
Ni kweli kwa macho ya nyama Mimi nimechoka
Wengi wanitazamapo kweli nimeshindwa
Wengi wanionavyo kweli nimeshindwa
Kweli kwa mbio za Mimi nimechoka
Kweli kwa mwendo wangu nimeshindwa
Kwa macho ya nyama nimechoka
Kwa macho ya watu nimeshindwa
Lakini hakuna hata mmoja
Anayejua patano langu na Mungu
Lakini hakuna hata mmoja anayejua nimepatana nini
Tumepatana na Baba hataniacha
Hata nikisukwa sukwa sitamuacha
Hata nikilia nisimuache
Hata nikiteseka aah nisimwache
Tumepatana na Baba
Nimepatana na Baba
Nimepatana na Baba
Nimepatana na Baba .
Naiona kesho yangu iliyonjema haa
Naiona kesho iliyonjema haa Mwenzenu
Naionaaaa kesho .
Naiona kesho kesho iliyopangwa na Baba (kesho ya heshima)
Naiona kesho kesho iliyopangwa na Mungu (kesho ya Neema)
Naiona kesho kesho iliyopangwa na Baba (kesho ya kufanikiwa)
Kesho ya heshima aah, kesho ya utukufu iliyopangwa na Baba
Kesho ya heshima (ya heshima yangu na mimi)
iliyopangwa na Mungu (kesho ya wote kumjua Mungu wangu)
Kesho ya heshima iliyopangwa na Baba
Kesho ya ushindi iliyopangwa na Mungu
Kesho ya utukufu wangu iliyopangwa na Baba
Kesho, kesho, kesho .