Chorus / Description :
Kwa moyo wangu wote
Nasema ahsante Kwako
Messiah nashukuru
Baba nashukuru
Umenipa uhai Baba
Nafasi nyingine ya siku mpya, Baba nashukuru
Umeniponya roho na mwili
tabibu wa ajabu ewe Yesu, Baba nashukuru
Umeondoa laana Baba,
Kabadilisha kuwa baraka, Baba nashukuru
Kilio changu ewe Yesu Kabadilisha kuwa furaha
Baba nashukuru
Kwa moyo wangu wote
Nasema ahsante Kwako
Messiah nashukuru
Nilipokuwa mnyonge Baba
Umekuwa nguvu yangu,Baba nashukuru
Nayo mishale ya yule mwovu
Haijanipata Umenilinda, Baba nashukuru
Umeniongoza Mwokozi wangu
Kanisimamisha imara, Baba nashukuru
Umenitoa kwenye shimo la giza
kanileta kwenye mwanga, Baba nashukuru
Kwa moyo wangu wote
Nasema ahsante Kwako
Messiah nashukuru
Yale yote umetenda
Ni mengi mno na ya ajabu
Sijui mimi nisemeje?
Yale Yahweh Umenitendea
Ni mengi mno na ya ajabu
Sijui mimi nisemeje?
Sijui mimi nisemeje? eeh
Kwa moyo wangu wote
Nasema ahsante Kwako
Messiah nashukuru