Chorus / Description :
Zangu zangu, Zangu zangu,
Zangu ni Shukrani Mungu
Nasifu Shani zako Elohim, safari mbali umenileta
Sina budi kuzishukuru hisani zako kuu.
Kwa ukarimu wako nabarikiwa
nitatoa nini kwako Bwana na vyote ni vyako
miye ni mlinzi ulivyoagiza Edeni..
Zangu zangu, Zangu zangu,
Zangu ni Shukrani Mungu
Sina neno uwapo karibu, nipatalolote si taabu,
Kifo na kaburi haviumi nitashinda kwako.
Nilalapo nikuone wewe, gizani mote nimulikiwe
nuru za mbinguni kweli hazikomi,
Siku zangu zote, kaa nami Bwana.
Zangu zangu, Zangu zangu,
Zangu ni Shukrani Mungu
Mapenzi yako sasa yatimie, wewe mfinyanzi mimi tope,
Unihojie dhambi zote, Unisafi Bwana.
Natoa vitu vyote kwako leo, maisha, mali, moyo vipokee,
mwili wangu wote ni Hekalu lako, Niongozee Bwana, N'takuimbia.
Zangu zangu, Zangu zangu,
Zangu ni Shukrani Mungu
#7thDayAdventist
#TheSaintsMinisters