Nikufananishe Na Nani Bwana Lyrics

By Lydia Odhiambo

Lyrics

Nikufananishe na nani Baba 

Nimetambua hufananishwi 


Uliumba mbingu kwa neno lako 

Ukaumba mji kwa neno lako 

Ulimwengu wote na vyote vilivyomo 

Vilikuwako kwa uwezo wako. 

Hapo mwanzo kulikuwako na neno 

Naye neno alikuwako kwa Mungu 

Naye neno alikuwa Mungu mwenyewe 

Nimetambua hufananishwi 


Nikufananishe na nani Bwana 

Nimetambua hufananishwi (*2) 


Umeinuliwa juu ya vyote Bwana 

Ufalme wako umetamalika 

Viumbe vyote vyakuabudu Jehovah 

Nimetambua hufananishwi 

Ndege angani wakusifu Bwana 

Samaki baharini wakuinua Jehovah 

Miti mimea zakuimbia wimbo mpya 

Nimetambua hufananishwi 


Nikufananishe na nani Bwana 

Nimetambua hufananishwi (*3) 


(Interlude) 


Nimekuona Baba ukiokoa wenye dhambi 

Ukiweka huru waliofungu 

Umewalisha wajane na watumwa 

Nimetambua hufananishwi 

Kwa jina lako mapepo hutoroka 

Kwa jina lako viwete watembea 

Kwa jina lako visiwi wasikia 

Nimetambua hufananishwi 


Nikufananishe na nani Bwana 

Nimetambua hufananishwi (*2) 


(Interlude 2) 


Nikufananishe na nani Bwana 

Nimetambua hufananishwi (*2) 


Now Playing...