Mwamba Wenye Imara
Lyrics
Mwamba wenye imara, kwako nitajificha!
maji hayo na damu, yaliyotoka humu,
hunisafi na dhambi, hunifanya mshindi
Kwa kazi zote pia , sitimizi sheria.
nijapofanya bidii, nikilia nakudhii,
hayaishi makosa: Ndiwe wa kuokoa.
Sina cha mkononi, Naja Msalabani;
Nili tupu, nivike; Ni mnyonge, nishike;
Nili mchafu naja, Nioshe nisijafa.
Nikungojapo chini, nakwenda kaburini;
nipaapo Mbinguni, na kukwona enzini;
roho yangu na iwe rahani mwako wewe.
Swahili version of Rock of Ages cleft for me
"Mwamba wenye Imara - Godwin Ombeni"
Song Information
- Artist
- Godwin Ombeni
- Released
- September 17, 2020
- Genre / Category
- swahili
- Views
- 3,884