1 Yohana Mlango 4 1st John

1 Yohana 4:1 1stJohn 4:1

Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.

1 Yohana 4:2 1stJohn 4:2

Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu.

1 Yohana 4:3 1stJohn 4:3

Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.

1 Yohana 4:4 1stJohn 4:4

Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia.

1 Yohana 4:5 1stJohn 4:5

Hao ni wa dunia; kwa hiyo wanena ya dunia na dunia huwasikia

1 Yohana 4:6 1stJohn 4:6

Sisi twatokana na Mungu. Yeye amjuaye Mungu atusikia; yeye asiyetokana na Mungu hatusikii. Katika hili twamjua Roho wa kweli, na roho ya upotevu.

1 Yohana 4:7 1stJohn 4:7

Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.

1 Yohana 4:8 1stJohn 4:8

Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo.

1 Yohana 4:9 1stJohn 4:9

Katika hili pendo la Mungu lilionekana kwetu, kwamba Mungu amemtuma Mwanawe pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kwa yeye.

1 Yohana 4:10 1stJohn 4:10

Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu.

1 Yohana 4:11 1stJohn 4:11

Wapenzi ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana.

1 Yohana 4:12 1stJohn 4:12

Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote. Tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu.

1 Yohana 4:13 1stJohn 4:13

Katika hili tunafahamu ya kuwa tunakaa ndani yake, naye ndani yetu, kwa kuwa ametushirikisha Roho wake.

1 Yohana 4:14 1stJohn 4:14

Na sisi tumeona na kushuhudia ya kuwa Baba amemtuma Mwana kuwa Mwokozi wa ulimwengu.

1 Yohana 4:15 1stJohn 4:15

Kila akiriye ya kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu.

1 Yohana 4:16 1stJohn 4:16

Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.

1 Yohana 4:17 1stJohn 4:17

Katika hili pendo limekamilishwa kwetu, ili tuwe na ujasiri katika siku ya hukumu; kwa kuwa, kama yeye alivyo, ndivyo tulivyo na sisi ulimwenguni humu.

1 Yohana 4:18 1stJohn 4:18

Katika pendo hamna hofu; lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu, kwa maana hofu ina adhabu; na mwenye hofu hakukamilishwa katika pendo.

1 Yohana 4:19 1stJohn 4:19

Sisi twapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza.

1 Yohana 4:20 1stJohn 4:20

Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona.

1 Yohana 4:21 1stJohn 4:21

Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.