Christ Ambassadors - Shukrani

Chorus / Description : Leo naamua kubadili mtazamo wangu Baba
Unajua muda mwingi nijapo mbele zako
Huwa naja nikilalamika
Lakini leo naleta shukrani shukrani
oh wastahili shukrani Baba

Shukrani Lyrics

Bwana wangu naomba unisikie  
Nijapo mbele zako 
(Naomba unisikie, naomba unisikie) 
Wimbo wangu siku ya leo si mwingine 
Bali ni wimbo wa shukrani 
(Bwana asante, kwa yote umenitendea) 

Leo naamua kubadili mtazamo wangu Baba 
Unajua muda mwingi nijapo mbele zako 
Huwa naja nikilalamika 
Lakini leo naleta shukrani shukrani 
oh wastahili shukrani Baba 

Muda wowote nikipatwa na jambo baya 
Siwezi sahau kulalamika 
(Kawaida ya mwanadamu, mwepesi wa kulalamika) 
Lakini kwa mazuri muda mwingi huwa nachukulia kawaida 
(Leo nakuja kwa sauti ya shukrani) 

Leo naamua kubadili mtazamo wangu Baba 
Unajua muda mwingi nijapo mbele zako 
Huwa naja nikilalamika 
Lakini leo naleta shukrani shukrani 
oh wastahili shukrani Baba 

Inapendeza kuja mbele zako 
Na sauti za shukrani ewe bwana wangu. 
(Inatupasa wanadamu kukushukuru daima) 
Ni vyema kuwa na shukrani nyingi 
kuliko malalamiko ooh oh. 
(Leo twakuja kwa sauti ya shukrani) 

Leo naamua kubadili mtazamo wangu Baba 
Unajua muda mwingi nijapo mbele zako 
Huwa naja nikilalamika 
Lakini leo naleta shukrani shukrani 
oh wastahili shukrani Baba 

Shukrani Video

  • Song: Shukrani
  • Artist(s): Christ Ambassadors


Share: