Chorus / Description :
Japo mengi hayajakwisha
Yatubidishayo tumshukuru Mungu wetu
Japo twapita majaribu mengi
Bado yapo mengi yakushukuriwa
Eeh ee jiunge nasi
Tulisisitize jambo hili la muhimu
Yale yote tujiulizayo moyoni
Majibu anayo Mungu wetu
Hebu tu tafakari
Mungu atutendeayo
Jinsi anavyo tujali
Jinsi anayo nilinda
Uhai wetu upitao tumsifu ungalipo
Ni ya ajabu sana
Matendo ya bwana Mungu
Kinachosikitisha hatuyadhamini kabisa
Lakini bwana ni mwema kwetu
Hawezi tuacha
Japo mengi hayajakwisha
Yatubidishayo tumshukuru Mungu wetu
Japo twapita majaribu mengi
Bado yapo mengi yakushukuriwa
Eeh ee jiunge nasi
Tulisisitize jambo hili la muhimu
Yale yote tujiulizayo moyoni
Majibu anayo Mungu wetu
Tuwapo safarini
Kifo kina tuandama
Tafakari safari zote
Kumbuka ile ajali
Ulifanya nini mpendwa ukatoka umzima
Ni ya ajabu sana
Matendo ya bwana Mungu
Kinachosikitisha hatuyadhamini kabisa
Lakini bwana ni mwema kwetu
Hawezi tuacha
Ni ya ajabu sana
Matendo ya bwana Mungu
Twapasa kushukuru kwa baraka anazotupa
Hakuna kitu wacha uhai ni yeye Mungu pekee
Tulalapo usiku
Twalala kama wafuu
Asubuhi kunapo kucha
Twadumu kuwa wazima
Ni ratiba yake tusifu
Ni mipango yake kwetu
Ni ya ajabu sana
Matendo ya bwana Mungu
Kinachosikitisha hatuyadhamini kabisa
Lakini bwana ni mwema kwetu
Hawezi tuacha
Ni ya ajabu sana
Matendo ya bwana Mungu
Twapasa kushukuru
Kwa baraka anazotupa
Hakuna kitu wacha uhai ni ye Mungu pekee
Ohh bwana ni mwema kwetu
Hawezi tuacha 3